1 John 2:15 — Compare Translations
14 translations compared side by side
Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Msiupende ulimwengu wala mambo yaliyo ulimwenguni. Mtu yeyote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Msiipende dunia hii ya uovu wala mambo yaliyomo ndani yake. Kama mkiipenda dunia, upendo wa baba haumo ndani yenu.
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Msiupende ulimwengu wala mambo yaliyoko ulimwenguni. Kama mtu ye yote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Msiupende ulimwengu wala mambo yaliyo ulimwenguni. Kama mtu yeyote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Msiupende ulimwengu huu, wala vilivyomo ulimwenguni! Mtu akiupenda ulimwengu huu, upendo wa Baba haumo mwake huyo.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Musipende dunia, wala mambo yanayokuwa katika dunia. Mutu akipenda dunia, hawezi kumupenda Mungu Baba.
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.