1 Peter 3:10 — Compare Translations

14 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Anayetaka kufurahia maisha, na kuona siku za fanaka, ajizuie asiseme mabaya aepe kusema uongo.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Kwa maana, “Yeyote apendaye uzima na kuona siku njema, basi auzuie ulimi wake usinene mabaya, na midomo yake isiseme hila.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Maandiko yanasema: “Anayetaka kufurahia maisha ya kweli na kuwa na siku nyingi njema tu, aepuke kusema chochote kinachoumiza, na asiruhusu uongo utoke kwenye kinywa yake.
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Anayetaka kufurahia maisha, na kuona siku za fanaka, anapaswa kuacha kusema mabaya na kuacha kusema uongo.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Anayetaka kufurahia maisha, na kuona siku za fanaka, ajizuie asiseme mabaya aepe kusema uongo.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Kwa maana, “Ye yote apendaye uzima na kuona siku njema, basi auzuie ulimi wake usinene mabaya na midomo yake isiseme hila.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Kwa maana, “Yeyote apendaye uzima na kuona siku njema, basi auzuie ulimi wake usinene mabaya, na midomo yake isiseme hila.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme uongo.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Anayetaka kufurahia maisha, na kuona siku za fanaka, ajizuie asiseme mabaya aepe kusema uongo.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Maana atakayependa kuwa uzimani naye atakaye kuona siku njema aulindie ulimi wake, usiseme mabaya, nayo midomo yake, isiseme madanganyifu!
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Kuna mutu anayependa kuishi vizuri, na kukaa katika siku za heri? Azuize ulimi wake na mabaya nayo midomo yake na uongo.
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Kwa maana, Atakae kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie nlimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila: