2 Samuel 21:19 — Compare Translations
11 translations compared side by side
Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Kulitokea tena mapigano na Wafilisti huko Gobu. Naye Elhanani mwana wa Yaareo-regimu, Mbethlehemu, alimuua Goliathi Mgiti, ambaye mpini wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumanguo.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, alimwua Goliathi, Mgiti, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Kulitokea tena mapigano na Wafilisti huko Gobu. Naye Elhanani mwana wa Yaareo-regimu, Mbethlehemu, alimuua Goliathi Mgiti, ambaye mpini wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumanguo.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Katika vita nyingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimwua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, alimwua Goliathi, Mgiti, ambaye mpini wa mkuki wake ulikuwa kama mpini wa mfuma nguo
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Kulitokea tena mapigano na Wafilisti huko Gobu. Naye Elhanani mwana wa Yaareo-regimu, Mbethlehemu, alimuua Goliathi Mgiti, ambaye mpini wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumanguo.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Kisha kule Gobu yakawa mapigano mengine na Wafilisti; ndiko, Elihanani wa Beti-Lehemu, mwana wa Yare-Orgimu, alikomwua Goliati wa Gati; huyu uti wa mkuki wake ulikuwa kama majiti ya wafuma nguo.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, alimwua Goliathi, Mgiti, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Kulitokea tena mapigano na Wafilistini kule Gobu. Elihanani mwana wa Yare-Oregimu, wa muji wa Betelehemu, alimwua Goliati wa muji wa Gati, ambaye mupini wa mukuki wake ulikuwa kama muti wa mufumaji wa nguo.