2 Samuel 21:4 — Compare Translations

11 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Wagibeoni wakamwambia, “Kisa chetu na Shauli pamoja na jamaa yake si jambo la fedha au dhahabu. Wala si juu yetu kumwua yeyote katika nchi ya Israeli.” Mfalme akawauliza tena, “Sasa mnasema niwatendee nini?”
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Na hao Wagibeoni wakamwambia, Si jambo la fedha wala dhahabu lililo kati ya sisi na Sauli, au nyumba yake; wala si juu yetu kumwua mtu ye yote katika Israeli. Akasema Mtakayoyanena, ndiyo nitakayowatendea ninyi.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Wagibeoni wakamwambia, “Kisa chetu na Shauli pamoja na jamaa yake si jambo la fedha au dhahabu. Wala si juu yetu kumwua yeyote katika nchi ya Israeli.” Mfalme akawauliza tena, “Sasa mnasema niwatendee nini?”
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumwua mtu ye yote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Na hao Wagibeoni wakamwambia, Si jambo la fedha wala dhahabu lililo kati ya sisi na Sauli, au nyumba yake; wala si juu yetu kumwua mtu yeyote katika Israeli. Akasema, Mtakayonena, ndiyo nitakayowatendea ninyi.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Wagibeoni wakamwambia, “Kisa chetu na Shauli pamoja na jamaa yake si jambo la fedha au dhahabu. Wala si juu yetu kumwua yeyote katika nchi ya Israeli.” Mfalme akawauliza tena, “Sasa mnasema niwatendee nini?”
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Wagibeoni wakamwambia: Sisi hatutaki fedha wala dhahabu kwake Sauli, wala kwao walio wa mlango wake, tena haitupasi kuua watu wa kwao Waisiraeli. Alipouliza tena: Mwasemaje? Niwafanyizie nini?
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Na hao Wagibeoni wakamwambia, Si jambo la fedha wala dhahabu lililo kati ya sisi na Sauli, au nyumba yake; wala si juu yetu kumwua mtu ye yote katika Israeli. Akasema Mtakayoyanena, ndiyo nitakayowatendea ninyi.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Wagibeoni wakamwambia: “Maneno kati yetu na Saulo pamoja na jamaa yake si jambo la kulipwa feza au zahabu, wala si jambo la kuua mutu yeyote katika inchi ya Israeli.” Mufalme akawauliza tena: “Sasa munasema niwatendee nini?”