Ecclesiastes 5:12 — Compare Translations
11 translations compared side by side
Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Usingizi wa kibarua ni mtamu, awe ameshiba au amekula kidogo tu. Lakini usingizi wa tajiri ni wa wasiwasi daima, maana ziada ya mali yake humsumbua usiku kucha.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Usingizi wa kibarua ni mtamu, awe amekula kidogo au kingi, lakini wingi wa mali humnyima tajiri usingizi.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Usingizi wake kibarua ni mtamu, kwamba amekula kidogo, au kwamba amekula kingi; lakini kushiba kwake tajiri hakumwachi kulala usingizi.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Usingizi wa kibarua ni mtamu, awe ameshiba au amekula kidogo tu. Lakini usingizi wa tajiri ni wa wasiwasi daima, maana ziada ya mali yake humsumbua usiku kucha.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Usingizi wa kibarua ni mtamu, awe amekula kidogo au kingi, lakini wingi wa mali humnyima tajiri usingizi.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Usingizi wa kibarua ni mtamu, awe amekula kidogo au kingi, lakini wingi wa mali humnyima tajiri usingizi.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Usingizi wake kibarua ni mtamu, awe amekula kidogo, au awe amekula kingi; lakini kushiba kwake tajiri hakumwachi kulala usingizi.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Usingizi wa kibarua ni mtamu, awe ameshiba au amekula kidogo tu. Lakini usingizi wa tajiri ni wa wasiwasi daima, maana ziada ya mali yake humsumbua usiku kucha.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Usingizi wa mtu wa kazi ni mtamu, kama anakula vichache au vingi; lakini shibe za mkwasi hazimpatii mapumziko ya kulala usingizi.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Usingizi wake kibarua ni mtamu, kwamba amekula kidogo, au kwamba amekula kingi; lakini kushiba kwake tajiri hakumwachi kulala usingizi.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Tena, nimeona jambo moja ovu sana chini ya jua: mutu alijikusanyia mali, ikakuwa hatari kwake.