Esther 2:7 — Compare Translations

9 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Alikuwa na binamu, Esta, ambaye jina lake la Kiebrania lilikuwa Hadasa. Esta alikuwa msichana mzuri wa sura na umbo. Wazazi wake walipofariki, Mordekai alimchukua Esta, akamlea kama binti yake.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Mordekai alikuwa na binamu yake msichana aliyeitwa Hadasa, ambaye alimlea kwa kuwa hakuwa na baba wala mama. Msichana huyu, ambaye pia alijulikana kwa jina la Esta, alikuwa na umbo na sura ya kupendeza, naye Mordekai alimtunza kama binti yake mwenyewe baada ya baba yake na mama yake kufariki.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Naye alikuwa amemlea Hadasa, yaani, Esta, binti wa mjomba wake, kwa kuwa hana baba wala mama. Naye msichana huyu alikuwa wa umbo mzuri na uso mwema; nao walipokufa baba yake na mama yake, yule Mordekai alimtwaa kuwa binti yake yeye.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Alikuwa na binamu, Esta, ambaye jina lake la Kiebrania lilikuwa Hadasa. Esta alikuwa msichana mzuri wa sura na umbo. Wazazi wake walipofariki, Mordekai alimchukua Esta, akamlea kama binti yake.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Mordekai alikuwa na binamu yake msichana aliyeitwa Hadasa, ambaye alimlea kwa kuwa hakuwa na baba wala mama. Msichana huyu, ambaye pia alijulikana kwa jina la Esta, alikuwa na umbo na sura ya kupendeza, naye Mordekai alimtunza kama binti yake mwenyewe baada ya baba yake na mama yake kufariki.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Mordekai alikuwa na binamu yake msichana aliyeitwa Hadasa, ambaye alimlea kwa kuwa hakuwa na baba wala mama. Msichana huyu, ambaye pia alijulikana kwa jina la Esta, alikuwa na umbo na sura ya kupendeza, naye Mordekai alimtunza kama binti yake mwenyewe baada ya baba yake na mama yake kufariki.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Yule alikuwa akimlea Hadasa (Kihagilo), ndiye Esteri (Nyota), binti wa mjomba wake, kwa sababu hakuwa na baba wala na mama. Huyu kijana wa kike alikuwa mwenye uso upendezao na mwenye mwili mzuri. Baba yake na mama yake walipokufa, Mordekai alimchukua, awe mwanawe.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Naye alikuwa amemlea Hadasa, yaani, Esta, binti wa mjomba wake, kwa kuwa hana baba wala mama. Naye msichana huyu alikuwa wa umbo mzuri na uso mwema; nao walipokufa baba yake na mama yake, yule Mordekai alimtwaa kuwa binti yake yeye.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Alikuwa anamulea binamu yake Hadasa ndiye Esteri. Esteri alikuwa binti muzuri wa sura na umbo. Wazazi wake walipokufa, Mordekayi akamutwaa Esteri, akamulea kama binti yake.