Exodus 29:5 — Compare Translations

11 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Kisha utachukua yale mavazi ya kikuhani umvike Aroni: Joho, kanzu, kizibao, kifuko cha kifuani, na kumfunga ule mshipi uliofumwa kwa ustadi.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Chukua yale mavazi na umvike Haruni koti, joho la kizibau, na kizibau chenyewe, pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kizibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Kisha twaa hayo mavazi na kumvika Haruni; itie kanzu, na joho ya naivera, na naivera, na kifuko cha kifuani, na kumkaza kwa huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi;
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Kisha utachukua yale mavazi ya kikuhani umvike Aroni: joho, kanzu, kizibao, kifuko cha kifuani, na kumfunga ule mshipi uliofumwa kwa ustadi.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Chukua yale mavazi na umvike Haruni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Kisha twaa hayo mavazi na kumvika Haruni; itie kanzu, na joho la naivera, na naivera, na kifuko cha kifuani, na kumkaza kwa huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi;
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Kisha utachukua yale mavazi ya kikuhani umvike Aroni: Joho, kanzu, kizibao, kifuko cha kifuani, na kumfunga ule mshipi uliofumwa kwa ustadi.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Kisha yachukue hayo mavazi, umvike Haroni shati na kanzu na kisibau na kibati cha kifuani, kisha umfunge kisibau kwa masombo ya kisibau.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Kisha twaa hayo mavazi na kumvika Haruni; itie kanzu, na joho ya naivera, na naivera, na kifuko cha kifuani, na kumkaza kwa huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi;
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Kisha utatwaa zile nguo za kikuhani umuvalishe Haruni: koti, kanzu, kizibao, kifuko cha kifua, na kumufunga ule mukaba uliofumwa kwa ufundi.