Ezekiel 18:14 — Compare Translations

11 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
“Lakini kama mtu huyo akiwa na mtoto ambaye ameona dhambi alizotenda baba yake, lakini yeye hatendi mabaya hayo,
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
“Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Na kama yeye huyo akizaa mwana, naye ameona dhambi zote za baba yake alizozitenda, akaogopa, asifanye neno lo lote kama hayo;
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
“Lakini kama mtu huyo akiwa na mtoto ambaye ameona dhambi alizotenda baba yake, lakini yeye hatendi mabaya hayo,
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
“Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
“Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Na kama yeye huyo akizaa mwana, naye ameona dhambi zote za baba yake alizozitenda, akaogopa, asifanye neno lolote kama hayo;
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
“Lakini kama mtu huyo akiwa na mtoto ambaye ameona dhambi alizotenda baba yake, lakini yeye hatendi mabaya hayo,
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Huyu akizaa mwana, naye akiyaona makosa yote, baba yake aliyoyatenda, lakini akiyaona tu, asiyafanye yaliyo kama hayo,
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Na kama yeye huyo akizaa mwana, naye ameona dhambi zote za baba yake alizozitenda, akaogopa, asifanye neno lo lote kama hayo;
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Lakini kama mutu yule akiwa na mutoto ambaye ameona zambi ambazo baba yake alitenda, lakini yeye hatendi mabaya yale, hatakufa juu ya uovu wa baba yake. Ni mutoto anayetenda hivi: hakuli sadaka kwenye milima, haziangalii sanamu za miungu ya Waisraeli, hamuchafui muke wa jirani yake, hamutendei mutu yeyote ubaya, hakamati rehani, haibi, anawapatia wenye njaa chakula na kuwavalisha wale wanaokuwa uchi, anaepuka kutenda uovu, anakopesha bila kudai faida wala kujipatia mazidio, anatii maagizo yangu na kufuata masharti yangu.