Genesis 37:22 — Compare Translations

11 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Msimwage damu. Ila mtumbukizeni katika shimo hili hapa mbugani, lakini msimdhuru.” Alisema hivyo kusudi aweze kumwokoa Yosefu mikononi mwao, na baadaye amrudishe kwa baba yake.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Msimwage damu yoyote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani mwa baba yake.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Reubeni akawaambia, Msimwage damu; mtupeni katika birika hii iliyopo nyikani, wala msimguse; ili apate kumwokoa katika mikono yao, akamrudishe kwa baba yake.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Msimwage damu. Ila mtumbukizeni katika shimo hili hapa mbugani, lakini msimdhuru.” Alisema hivyo kusudi aweze kumwokoa Yosefu mikononi mwao, na baadaye amrudishe kwa baba yake.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Tusimwage damu yo yote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani kwa baba yake.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Tusimwage damu yoyote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani kwa baba yake.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Reubeni akawaambia, Msimwage damu; mtupeni katika shimo hili lililopo nyikani, wala msimguse; ili apate kumwokoa katika mikono yao, akamrudishe kwa baba yake.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Msimwage damu. Ila mtumbukizeni katika shimo hili hapa mbugani, lakini msimdhuru.” Alisema hivyo kusudi aweze kumwokoa Yosefu mikononi mwao, na baadaye amrudishe kwa baba yake.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Kisha Rubeni akawaambia: Msimwage damu yake! Mtupeni humu shimoni huku nyikani! Lakini msimwue kwa kumpelekea mikono! Naye alisema hivyo, apate kumponya mikononi mwao, amrudishe kwa baba yake.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Reubeni akawaambia, Msimwage damu; mtupeni katika birika hii iliyopo nyikani, wala msimguse; ili apate kumwokoa katika mikono yao, akamrudishe kwa baba yake.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Musimwange damu. Mumutumbukize katika shimo hili hapa katika mbuga, lakini musimuzuru.” Alisema hivyo kusudi aweze kumwokoa Yosefu kutoka mikono yao na kisha amurudishe kwa baba yake.