Isaiah 39:8 — Compare Translations
11 translations compared side by side
Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Naye Hezekia akamwambia Isaya, “Neno la Mwenyezi-Mungu ulilosema ni sawa.” Alisema hivyo kwani alifikiri, “Kutakuwa na amani na usalama muda wote niishipo.”
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Mwenyezi Mungu ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Kutakuwa amani na usalama wakati wa uhai wangu.”
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Ndipo Hezekia akamwambia Isaya, Neno la Bwana ulilolinena ni jema. Tena akamwambia, Maana itakuwapo amani na kweli katika siku zangu mimi.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Naye Hezekia akamwambia Isaya, “Neno la Mwenyezi-Mungu ulilosema ni sawa.” Alisema hivyo kwani alifikiri, “Kutakuwa na amani na usalama muda wote niishipo.”
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Hezekia akajibu, “Neno la BWANA ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Patakuwepo amani na salama katika siku za maisha yangu.”
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Patakuwepo amani na usalama wakati wa uhai wangu.”
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Ndipo Hezekia akamwambia Isaya, Neno la BWANA ulilolinena ni jema. Tena akamwambia, Maana alifikiri, kutakuwapo na amani na usalama katika siku zangu mimi.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Naye Hezekia akamwambia Isaya, “Neno la Mwenyezi-Mungu ulilosema ni sawa.” Alisema hivyo kwani alifikiri, “Kutakuwa na amani na usalama muda wote niishipo.”
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Hizikia akamwambia Yesaya: Neno la Bwana, ulilolisema, ni jema, kwani alisema moyoni: Katika siku zangu utakuwako utengemano wa kweli.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Ndipo Hezekia akamwambia Isaya, Neno la BWANA ulilolinena ni jema. Tena akamwambia, Maana itakuwapo amani na kweli katika siku zangu mimi.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Naye Hezekia akamwambia Isaya: Neno la Yawe ulilosema ni zuri. Alisema hivyo maana alifikiri: Kutakuwa amani na salama muda wote wa maisha yangu.