Isaiah 63:1 — Compare Translations
11 translations compared side by side
Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Ni nani huyu ajaye kutoka Edomu, anayefika kutoka Bosra na mavazi ya madoa mekundu? Ni nani huyo aliyevaa mavazi ya fahari, anatembea kwa nguvu zake kubwa? Ni mimi Mwenyezi-Mungu ninayetangaza ushindi wangu; nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Ni nani huyu atokaye Edomu, Mwenye mavazi ya kutiwa damu kutoka Bosra? Huyu aliye na nguo za fahari, Anayekwenda katika ukuu wa uweza wake?
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Ni nani huyu ajaye kutoka Edomu, anayefika kutoka Bosra na mavazi ya madoa mekundu? Ni nani huyo aliyevaa mavazi ya fahari, anatembea kwa nguvu zake kubwa? Ni mimi Mwenyezi-Mungu ninayetangaza ushindi wangu; nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Ni nani huyu atokaye Edomu, Atokaye Bosra akiwa na mavazi yenye madoa mekundu? Huyu aliye na nguo za fahari, Anayekwenda katika ukuu wa uweza wake? Ndimi nisemaye kwa haki, Niliye hodari wa kuokoa.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Ni nani huyu ajaye kutoka Edomu, anayefika kutoka Bosra na mavazi ya madoa mekundu? Ni nani huyo aliyevaa mavazi ya fahari, anatembea kwa nguvu zake kubwa? Ni mimi Mwenyezi-Mungu ninayetangaza ushindi wangu; nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Ni nani huyu anayetoka Edomu na kuvaa nguo nyekundu za Bosira? Ni mtukufu katika vazi lake, anatembea na kuzionyesha nguvu zake nyingi; anasema: Yuko nani asemaye kwa wongofu? Ninazo njia nyingi za kuokoa.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Ni nani huyu atokaye Edomu, Mwenye mavazi ya kutiwa damu kutoka Bosra? Huyu aliye na nguo za fahari, Anayekwenda katika ukuu wa uweza wake? Mimi nisemaye kwa haki, Hodari wa kuokoa.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, anayefika kutoka Bosira na nguo ya madoa mekundu? Ni nani huyo aliyevaa nguo ya utukufu, anatembea kwa nguvu zake kubwa? Ni mimi Yawe ninayetangaza ushindi wangu; nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.