Joel 2:5 — Compare Translations

11 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Wanaporukaruka kwenye vilele vya milima, wanarindima kama magari ya farasi, wanavuma kama mabua makavu motoni. Wamejipanga kama jeshi kubwa tayari kabisa kufanya vita.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Wanatoa sauti kama magari ya vita, wanaporukaruka juu ya vilele vya milima, kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua, kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Kama mshindo wa magari ya vita juu ya vilele vya milima, ndivyo warukavyo; kama mshindo wa miali ya moto ilapo mabua makavu, kama mashujaa waliopangwa tayari kwa vita.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Wanaporukaruka kwenye vilele vya milima, wanarindima kama magari ya farasi, wanavuma kama mabua makavu motoni. Wamejipanga kama jeshi kubwa tayari kabisa kufanya vita.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Wanatoa sauti kama magari ya vita, wanaporukaruka juu ya vilele vya milima, kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua, kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Wanatoa sauti kama magari ya vita, wanaporukaruka juu ya vilele vya milima, kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua, kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Kama mshindo wa magari ya vita juu ya vilele vya milima, ndivyo warukavyo; kama mshindo wa miali ya moto iunguzapo mabua makavu, kama mashujaa waliopangwa tayari kwa vita.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Wanaporukaruka kwenye vilele vya milima, wanarindima kama magari ya farasi, wanavuma kama mabua makavu motoni. Wamejipanga kama jeshi kubwa tayari kabisa kufanya vita.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Uvumi wao ni kama wa magari yarukayo milimani juu au kama uvumi wa moto ulao majani makavu; ni kama wa watu wenye nguvu waliojipanga kupigana.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Kama mshindo wa magari ya vita juu ya vilele vya milima, ndivyo warukavyo; kama mshindo wa miali ya moto ilapo mabua makavu, kama mashujaa waliopangwa tayari kwa vita.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Wanaporukaruka kwenye vilele vya milima, wananguruma kama magari yenye kukokotwa na farasi, wanavuma kama moto wa majani yenye kukauka. Wamejipanga kama kundi kubwa la waaskari tayari kabisa kufanya vita.