John 5:7 — Compare Translations

14 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Naye akajibu, “Bwana, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia.”
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana, mimi sina mtu wa kuniingiza bwawani maji yanapotibuliwa. Nami ninapotaka kutumbukia bwawani, mtu mwingine huingia kabla yangu.”
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; ila wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu.
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Yule mgonjwa akajibu, “Bwana, hakuna mtu wa kunisaidia kuingia kwenye bwawa mara maji yanapotibuliwa. Najitahidi kuwa wa kwanza kuingia majini. Lakini ninapojaribu, mtu mwingine huniwahi na kuingia majini kabla yangu.”
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Naye akajibu, “Mheshimiwa, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia.”
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Naye akajibu, “Bwana, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia.”
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana, mimi sina mtu wa kuniingiza bwawani maji yanapotibuliwa. Nami ninapotaka kutumbukia bwawani, mtu mwingine huingia kabla yangu.”
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana, mimi sina mtu wa kuniingiza bwawani maji yanapotibuliwa. Nami ninapotaka kutumbukia bwawani, mtu mwingine huingia kabla yangu.”
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina mtu wa kunitia katika bwawa, maji yanapotibuliwa; ila wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Naye akajibu, “Bwana, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia.”
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Mgonjwa akamjibu: Bwana, sina mtu wa kunitia kiziwani, maji yanapotikiswa. Kila mara mimi ninapokwenda, mwingine hushuka mbele yangu.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; ila wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Yule mugonjwa akamujibu: “Bwana, sina mutu wa kuniingiza katika kisima wakati maji yanapotikiswa, nami ninapojaribu kuingia ndani ya maji, mutu mwingine anaingia mbele yangu.”
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; bali wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu.