Leviticus 20:6 — Compare Translations
11 translations compared side by side
Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
“Kama mtu yeyote anawaendea waaguzi wa mizimu na wachawi na hivyo kukosa uaminifu kwangu, nitamkabili mtu huyo na kumtenga na watu wake.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
“ ‘Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu anayeenda kwa waaguzi na wenye pepo, na hivyo kujifanyia ukahaba kwa kuwafuata, nami nitamkatilia mbali na watu wake.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Na mtu yule atakayewaendea wenye pepo, na wachawi, ili kuzini pamoja nao, nitakaza uso wangu juu ya mtu yule, nitamtenga na watu wake.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
“Kama mtu yeyote anawaendea waaguzi wa mizimu na wachawi na hivyo kukosa uaminifu kwangu, nitamkabili mtu huyo na kumtenga na watu wake.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
“ ‘Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu anayewaendea waaguzi na wenye pepo kwa kujifanyia ukahaba kwa kuwafuata, nami nitamkatilia mbali na watu wake.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
“ ‘Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu anayeenda kwa waaguzi na wenye pepo, na hivyo kujifanyia ukahaba kwa kuwafuata, nami nitamkatilia mbali na watu wake.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Na mtu yule atakayewaendea wenye pepo, na wachawi, ili kuzini pamoja nao, nitakaza uso wangu juu ya mtu yule, nitamtenga na watu wake.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
“Kama mtu yeyote anawaendea waaguzi wa mizimu na wachawi na hivyo kukosa uaminifu kwangu, nitamkabili mtu huyo na kumtenga na watu wake.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Hata mtu akiwageukia waganga wa kutiisha mizimu na waaguaji, kufanya ugoni nao, na nimkazie macho yangu aliye hivyo, na nimg'oe katikati yao walio ukoo wake.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Na mtu yule atakayewaendea wenye pepo, na wachawi, ili kuzini pamoja nao, nitakaza uso wangu juu ya mtu yule, nitamtenga na watu wake.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Kama mutu yeyote anawaendea waaguzi wa mizimu na wachawi na hivyo kukosa uaminifu kwangu, nitamukasirikia mutu huyu na kumutenga na watu wake.