Luke 2:40 — Compare Translations

14 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa naye.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akijawa na hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Mtoto Yesu aliendelea kukua na kuwa kijana mwenye nguvu na aliyejaa hekima nyingi. Na Mungu alikuwa anambariki.
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa naye.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Naye mtoto Yesu akakua na kuongezeka nguvu akiwa amejaa hekima na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa naye.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Lakini yule mtoto akakua, akapata nguvu ya Roho na werevu wote wa kweli, naye Mungu akamgawia mema yake.*
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Mutoto yule akakomaa, akazidi kuwa na nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Mtoto yule akakua, akaongezeka nguvu, akajazwa hekima; neema ya Mungu ikawa pamoja nae.