Luke 4:20 — Compare Translations

14 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Yesu akalivingirisha gombo akalifunga, akalirudisha kwa msaidizi na kuketi chini. Kwa kuwa kila mtu ndani ya sinagogi alimwangalia kwa makini,
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi, akaketi. Ndipo, wote waliokuwamo humo nyumbani mwa kuombea walipomkazia macho,
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Kisha akafunga kile kitabu, akakipatia mutumishi wa nyumba ya kuabudia na kuikaa. Na watu wote waliokuwa ndani ya ile nyumba ya kuabudia wakamukazia macho.
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Akakifunga chuo, akampa mkhudumu, akaketi: watu wote waliokuwa katika sunagogi wakamkazia macho.