Luke 4:36 — Compare Translations
14 translations compared side by side
Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, “Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!”
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Mshangao ukawashika wote, wakasemezana wakisema, Ni neno gani hili, maana awaamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu, nao hutoka.
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Watu wakashangaa. Wakasemezana wao kwa wao, “Hii inamaanisha nini? Kwa mamlaka na uwezo anaamuru pepo wachafu na wanatoka!”
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, “Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!”
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, “Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!”
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Watu wote wakashangaa wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Kwa mamlaka na nguvu, anawaamuru pepo wachafu, nao wanatoka!”
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Mshangao ukawashika wote, wakasemezana wakisema, Ni neno gani hili, maana awaamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu, nao hutoka.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, “Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!”
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Wote wakaingiwa na kituko, wakasemezana wao kwa wao wakiuliza: Neno gani hilo? Anawaagiza pepo wachafu kwa nguvu ya kifalme, nao hutoka!
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Mshangao ukawashika wote, wakasemezana wakisema, Ni neno gani hili, maana awaamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu, nao hutoka.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Watu wote wakashangaa sana na kusemezana: “Hatujaona mambo kama haya! Mutu huyu anawaamuru pepo kwa mamlaka na uwezo wake, nao wanatoka!”
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Ushangao ukawashika wote, wakaambiana wao kwa wao, wakinena, Neno gani hili, maana kwa mamlaka na uweza awaamuru pepo wachafu, nao watoka?