Mark 8:4 — Compare Translations

14 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Wanafunzi wake wakamwuliza, “Hapa nyikani itapatikana wapi mikate ya kuwashibisha watu hawa wote?”
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Wanafunzi wake wakamjibu, Je! Ataweza wapi mtu kuwashibisha hawa mikate hapa nyikani?
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Wanafunzi wake wakamjibu, “Wapi mtu yeyote atapata chakula cha kutosha mahali hapa jangwani cha kuwalisha watu hawa?”
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Wanafunzi wake wakamwuliza, “Hapa nyikani itapatikana wapi mikate ya kuwashibisha watu hawa wote?”
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Wanafunzi wake wakamwuliza, “Hapa nyikani itapatikana wapi mikate ya kuwashibisha watu hawa wote?”
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Wanafunzi wake wakamjibu, Je! Ataweza wapi mtu kuwashibisha hawa mikate hapa nyikani?
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Wanafunzi wake wakamwuliza, “Hapa nyikani itapatikana wapi mikate ya kuwashibisha watu hawa wote?”
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Wanafunzi wake walipomjibu: Hapa nyikani mtu atawezaje kuwashibisha watu hawa mikate?
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Wanafunzi wake wakamjibu, Je! Ataweza wapi mtu kuwashibisha hawa mikate hapa nyikani?
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Wanafunzi wake wakamujibu: “Hapa katika pori mutu ataweza kupata wapi chakula cha kuwashibisha?”
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Wanafunzi wake wakamjibu, Atawezaje mtu kuwashibisha hawa mikate hapa nyikani?