Mark 9:35 — Compare Translations
14 translations compared side by side
Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Yesu akaketi chini, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia, “Mtu akitaka kuwa wa kwanza lazima awe wa mwisho na mtumishi wa wote.”
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Akaketi chini, akawaita wote kumi na wawili, akawaambia: “Kama mtu yeyote akitaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa wa mwisho na mtumishi wa wote.”
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Akaketi chini, akawaita wale Thenashara akawaambia, Mtu atakaye kuwa wa kwanza atakuwa wa mwisho kuliko wote, na mtumishi wa wote.
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Hivyo Yesu aliketi chini, akawaita wale kumi na mbili, na akawaambia, “Ikiwa yupo mtu yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, inapasa basi awe wa mwisho kuliko wote na mtumishi wa wote.”
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Yesu akaketi chini, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia, “Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza lazima awe wa mwisho na kuwa mtumishi wa wote.”
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Yesu akaketi chini, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia, “Mtu akitaka kuwa wa kwanza lazima awe wa mwisho na mtumishi wa wote.”
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Akaketi, akawaita wote kumi na wawili akawaambia: “Kama mtu ye yote akitaka kuwa wa kwanza hana budi kuwa wa mwisho na mtumishi wa wote.”
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Akaketi chini, akawaita wote kumi na wawili, akawaambia: “Kama mtu yeyote akitaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa wa mwisho na mtumishi wa wote.”
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Akaketi chini, akawaita wale Kumi na Wawili akawaambia, Mtu atakaye kuwa wa kwanza atakuwa wa mwisho kuliko wote, na mtumishi wa wote.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Yesu akaketi chini, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia, “Mtu akitaka kuwa wa kwanza lazima awe wa mwisho na mtumishi wa wote.”
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Akakaa, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia: Mtu akitaka kuwa wa kwanza, sharti awafuate wenzake wote nyuma, awe mtumishi wao wote!
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Akaketi chini, akawaita wale Thenashara akawaambia, Mtu atakaye kuwa wa kwanza atakuwa wa mwisho kuliko wote, na mtumishi wa wote.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Basi Yesu akaikaa, akawaita wanafunzi wake kumi na wawili na kuwaambia: “Mutu anayetaka kuwa wa kwanza anapaswa kujiweka wa mwisho kuliko wote na kuwa mutumishi wa wote.”
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Akaketi chini akawaita wathenashara akawaambia, Mtu atakae kuwa wa kwanza atakuwa wa mwisho kuliko wote, na mkhudumu wa wote.