Mark 9:8 — Compare Translations
14 translations compared side by side
Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Mara wanafunzi hao wakatazama tena, lakini hawakumwona mtu mwingine, ila Yesu peke yake pamoja nao.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Mara walipotazama huku na huku, hawakuona tena mtu mwingine yeyote pamoja nao isipokuwa Isa.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Mara hiyo walipotazama huku na huku, hawakuona mtu pamoja nao ila Yesu peke yake.
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Ndipo ghafula walipokuwa wakiangalia huku na huko, hawakuona mtu yeyote akiwa pamoja nao isipokuwa Yesu peke yake.
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Mara wanafunzi hao wakatazama tena, lakini hawakumwona mtu mwingine, ila Yesu peke yake pamoja nao.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Mara wanafunzi hao wakatazama tena, lakini hawakumwona mtu mwingine, ila Yesu peke yake pamoja nao.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Mara walipotazama huku na huku, hawakuona tena mtu mwingine ye yote pamoja nao isipokuwa Yesu.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Mara walipotazama huku na huku, hawakuona tena mtu mwingine yeyote pamoja nao isipokuwa Isa.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Mara hiyo walipotazama huku na huku, hawakuona mtu pamoja nao ila Yesu peke yake.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Mara wanafunzi hao wakatazama tena, lakini hawakumwona mtu mwingine, ila Yesu peke yake pamoja nao.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Mara walipotazama huko na huko, hakuna waliyemwona, asipokuwa Yesu peke yake pamoja nao.
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Mara hiyo walipotazama huku na huku, hawakuona mtu pamoja nao ila Yesu peke yake.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Mara moja wanafunzi waliangalia pande zao zote, hawakumwona mutu mwingine pamoja nao, isipokuwa Yesu peke yake.
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Na marra hiyo walipotazama huku na huku, hawakumwona mtu, illa Yesu peke yake pamoja nao.