Matthew 20:22 — Compare Translations

14 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Isa akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe nitakachonywea mimi?” Wakajibu, “Tunaweza.”
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Hivyo Yesu akawaambia wana wa Zebedayo, “Hamwelewi mnachokiomba. Mnaweza kukinywea kikombe ambacho ni lazima nikinywee?” Wana wa Zebedayo wakajibu, “Ndiyo tunaweza!”
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloomba. Je, ninyi mnaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi?” Wakajibu, “Tunaweza.”
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Isa akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe nitakachonywea mimi?” Wakajibu, “Tunaweza.”
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Yesu akajibu akisema: Hamjui mnaloliomba. Mwaweza kukinywa kinyweo, nitakachokinywa mimi? Walipomwambia: Twaweza,
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Yesu akawaambia: “Hamujui kitu munachoomba. Munaweza kubeba muzigo wa mateso nitakaoubeba?” Nao wakamujibu: “Tunaweza.”
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomha. Mwaweza kuuywea kikombe nitakachonywea mimi, na kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi? Wakamwambia, Twaweza.