Nahum 2:12 — Compare Translations

11 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Simba dume amewararulia watoto wake nyama ya kutosha, akawakamatia simba majike mawindo yao; ameyajaza mapango yake mawindo, na makao yake mapande ya nyama.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Simba aliua mawindo ya kutosha watoto wake, alinyonga mawindo kwa ajili ya mwenzi wake, akijaza makao yake kwa alivyoua na mapango yake kwa mawindo.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Simba alirarua vipande vipande chakula cha kuwatosha watoto wake, aliwasongea wake zake nyama, aliyajaza mapango yake mateka, na makao yake aliyajaza mawindo.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Simba dume amewararulia watoto wake nyama ya kutosha, akawakamatia simba majike mawindo yao; ameyajaza mapango yake mawindo, na makao yake mapande ya nyama.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Simba aliua mawindo ya kutosha watoto wake, alinyonga mawindo kwa ajili ya mwenzi wake, akijaza makao yake kwa alivyoua na mapango yake kwa mawindo.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Simba aliua mawindo ya kutosha watoto wake, alinyonga mawindo kwa ajili ya mwenzi wake, akijaza makao yake kwa alivyoua na mapango yake kwa mawindo.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Simba alirarua vipande vipande chakula cha kuwatosha watoto wake, aliwakamatia majike wake mawindo, aliyajaza mapango yake mateka, na makao yake aliyajaza nyama iliyoraruliwa.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Simba dume amewararulia watoto wake nyama ya kutosha, akawakamatia simba majike mawindo yao; ameyajaza mapango yake mawindo, na makao yake mapande ya nyama.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Makao ya simba yako wapi? Malisho ya wana wa simba yako wapi nayo? Ndipo wapi, walipotembea simba mume na mke na watoto pasipo kuona awastushaye?
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Simba alirarua vipande vipande chakula cha kuwatosha watoto wake, aliwasongea wake zake nyama, aliyajaza mapango yake mateka, na makao yake aliyajaza mawindo.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Basi lile pango la simba limekuwa namna gani, lile lililokuwa maficho ya simba wakali? Ile nafasi ya simba imekuwa namna gani, nafasi ya wana-simba ambayo hakuna aliyeweza kuwashitua?