Romans 3:28 — Compare Translations

14 translations compared side by side

Swahili (BHN) (Habari Njema) 2001
Maana Mungu humkubali mtu kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya sheria.
Swahili (Neno: Maandiko Matakatifu 2024)
Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kupitia kwa imani wala si kwa matendo ya sheria.
Swahili (SRUV) (Swahili Revised Union Version)
Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
Swahili (TKU) 2017 (Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi)
Ninamaanisha kuwa watu hufanyika wenye haki na kukubaliwa na Mungu kwa njia ya imani, siyo kwa sababu ya yale wanayotenda ili kuifuata sheria. Hili ndilo tunaloamini.
Swahili 1850 - Biblia Takatifu
Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
Swahili BHNTLK (Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza)
Maana Mungu humkubali mtu kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya sheria.
Swahili NEN (Neno: Bibilia Takatifu 2025)
Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
Swahili RSUVDC (BIBLIA KISWAHILI)
Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
Swahili SCLDC10 (BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA)
Maana Mungu humkubali mtu kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya sheria.
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
Kwani tunalishika hili la kwamba: Mtu hupata wongofu kwa kumtegemea Mungu tu, ijapo asiyatimize Maonyo.*
Swahili SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Kwa maana tunaona kama mutu anahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani wala si kwa njia ya kutii Sheria.
Swahili SWZZB1921 (New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921)
Bassi, twahasibu ya kuwa mwana Adamu hupewa baki kwa imani pasipo matendo ya sharia.