bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Samuel 29
1 Samuel 29
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 28
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 30 →
1
Wafilistini walikusanya makundi yao yote ya waaskari kule Afeki, na Waisraeli walipiga kambi kwenye chemichemi ya bonde la Yezereheli.
2
Wakubwa watano wa Wafilistini walipokuwa wakipita na makundi yao ya waaskari ya mamia na maelfu, Daudi naye akiwa na watu wake pamoja na Akisi walikuwa wanafuata upande wa nyuma wa kundi lile.
3
Wakubwa wa waaskari wa Wafilistini waliuliza: “Waebrania hawa wanafanya nini hapa?” Akisi akawajibu wale wakubwa wa Wafilistini: “Huyu ni Daudi, mutumishi wa Saulo mufalme wa Israeli; naye amekuwa nami kwa miaka fulani. Na tangu alipokimbilia kwangu, sijamupata na kosa lolote.”
4
Lakini wakubwa wa Wafilistini walimukasirikia sana Akisi, wakamwambia: “Umurudishe aende pahali ulipomupa akae. Asiende hata kidogo pamoja nasi kwa vita, kama sivyo wakati wa vita atageuka na kuwa adui yetu. Hauoni kwamba mutu huyu atapata njia nzuri ya kupatana na bwana wake halafu kuwa adui yetu katika vita?
5
Huyu ni Daudi yuleyule ambaye wanawake waliimba habari zake walipokuwa wakicheza: ‘Saulo ameua maelfu, lakini Daudi ameua maelfu kumi.’ ”
6
Akisi akamwita Daudi na kumwambia: “Kama vile Yawe anavyoishi, umekuwa mutu wa usawa. Ingekuwa jambo zuri kwangu tuende wote katika vita, kwa maana sijaona jambo baya lolote kwako tangu siku ile ulipokuja kwangu mpaka leo hii. Hata hivyo, wakubwa hawajapendezwa nawe.
7
Hivyo sasa, urudi kwa nyumba. Kwenda kwa amani kusudi usiwachukize wakubwa wa Wafilistini.”
8
Daudi akamwambia Akisi: “Lakini nimefanya nini? Kama unavyosema kwamba haujaniona na kosa lolote tangu siku ile nilipoanza kukutumikia mpaka leo, kwa nini nisiende kupigana na waadui za bwana wangu mufalme?”
9
Akisi akamwambia: “Ninajua kwamba hauna lawama mbele yangu kama malaika wa Mungu. Hata hivyo, wakubwa wa Wafilistini wamesema: ‘Asiende hata kidogo pamoja nasi katika vita’.
10
Sasa, wewe pamoja na watumishi wa bwana wako Saulo waliokuja pamoja nawe, kesho asubui mapema, muamuke na kuondoka mara tu kunapopambazuka.”
11
Kwa hiyo, kesho yake asubui, Daudi pamoja na watu wake waliondoka kurudi katika inchi ya Wafilistini. Lakini hao Wafilistini wakaenda Yezereheli.
← Chapter 28
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 30 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31