bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Samuel 8
1 Samuel 8
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 7
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 9 →
1
Samweli alipokuwa muzee, aliwafanya wana wake kuwa waamuzi wa Waisraeli.
2
Mwana wake wa kwanza aliitwa Yoeli, na wa pili aliitwa Abiya. Wote wawili walikuwa waamuzi kule Beri-Seba.
3
Lakini watoto hao hawakufuata mwenendo wa baba yao. Lakini walianza kujitafutia faida. Wakapokea kituliro na kupotosha haki.
4
Basi, viongozi wote wa Waisraeli walikusanyika pamoja, na kumwendea Samweli katika muji wa Rama,
5
wakamwambia: “Angalia, wewe sasa ni muzee na watoto wako hawafuati mwenendo wako. Hivyo, utuchagulie mufalme wa kututawala sawa vile inavyokuwa kwa mataifa mengine.”
6
Lakini jambo la Waisraeli la kutaka wapewe mufalme wa kuwatawala, halikumupendeza Samweli. Naye akamwomba Yawe.
7
Yawe akamwambia: “Sikiliza kila kitu ambacho watu wanakuambia; maana hawajakukataa wewe, lakini wamenikataa mimi kuwa mufalme juu yao.
8
Tangu nilipowatoa Misri, wameniacha mimi, wamekuwa wakiitumikia miungu mingine mpaka leo. Sasa hayo matendo ambayo wamekuwa wakinitendea mimi, ndiyo wanayokutendea na wewe.
9
Basi, uwasikilize, lakini uwaonye vikali, na uwaelezee waziwazi jinsi mufalme atakayewatawala atakavyowatendea.”
10
Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wanaomba wapewe mufalme maneno yote ya Yawe.
11
Samweli aliwaambia: “Hivi ndivyo mufalme wenu atakayewatawala atakavyowatendea: wana wenu atawafanya wakuwe waendeshaji wa magari yake, na wengine kuwa waaskari wapanda-farasi wake, na wengine watapiga mbio mbele ya magari yake.
12
Atajichagulia wengine wakuwe wakubwa wa makundi ya waaskari wake wa maelfu na wengine wakuwe wakubwa wa makundi ya watu makumi tano. Atawafanya wengine wamulimie mashamba yake na kuvuna mazao yake. Atawafanya wengine vilevile wamutengenezee silaha za vita, na wengine wamutengenezee vyombo vya magari yake.
13
Wabinti zenu atawatwaa kuwa watengenezaji wa marasi, wengine wapishi na wengine wachomaji wa mikate.
14
Atayatwaa mashamba yenu mazuri, mashamba ya mizeituni, na mashamba ya mizabibu na kuwapa watumishi wake.
15
Atatwaa sehemu ya kumi ya ngano zenu na ya zabibu zenu na kuwapa wakubwa wake na watumishi wake.
16
Atatwaa watumishi wenu na wajakazi wenu na ngombe wenu wazuri na punda wenu wazuri kabisa na kuwafanya wamufanyie kazi yake.
17
Atatwaa sehemu ya kumi ya kondoo wenu. Na ninyi wenyewe mutakuwa watumwa wake.
18
Wakati huo, ninyi mutalalamika kwa sababu ya mufalme wenu ambaye mumejichagulia ninyi wenyewe. Lakini Yawe hatawajibu.”
19
Hata hivyo watu walikataa kumusikiliza Samweli, wakasema: “Hapana! Sisi tutakuwa na mufalme juu yetu,
20
kusudi nasi vilevile tukuwe sawa mataifa mengine. Mufalme wetu, atatuamulia haki zetu, atatuongoza na kutupigania vita vyetu.”
21
Samweli alipokwisha kusikiliza kila kitu walichosema, akaenda na kumwelezea Yawe.
22
Yawe akamwambia Samweli: “Uwasikilize na uwapatie mufalme.” Kisha Samweli akawaambia Waisraeli warudie kwao, kila mutu katika muji wake.
← Chapter 7
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 9 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31