bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Corinthians 3
2 Corinthians 3
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 4 →
1
Maneno haya yanaonyesha kwamba tunaanza kujisifu tena sisi wenyewe? Au tunahitaji kuwatolea ninyi barua za ushuhuda au kuziomba kwenu kama wengine?
2
Ninyi wenyewe ni kama barua yetu ya ushuhuda iliyoandikwa katika mioyo yetu na watu wote wanaweza kuitambua na kuisoma.
3
Inaonekana wazi kwamba ninyi ni barua iliyoandikwa na Kristo na kutumwa kwa njia ya utumishi wetu. Barua hii inaandikwa si kwa wino, lakini kwa Roho wa Mungu Mwenye Uzima. Barua hiyo haikuandikwa juu ya vibao vya mawe, lakini katika mioyo ya watu.
4
Tunasema neno hili kwa ajili ya tumaini tunalokuwa nalo kwa Mungu kwa njia ya Kristo.
5
Si kusema kwamba sisi wenyewe tuko na uwezo wa kujitungia jambo hili, lakini uwezo wetu unatoka kwa Mungu.
6
Kwa maana Mungu ndiye aliyetuwezesha kuwa watumishi wa agano jipya, lisilotokana na Sheria iliyoandikwa, lakini na Roho. Sheria iliyoandikwa inaleta kifo lakini Roho analeta uzima.
7
Sheria ile inayoleta kifo imeandikwa neno kwa neno juu ya vibao vya mawe na utukufu wa Mungu ulingaa wakati ule. Uso wa Musa ukangaa vilevile hata Waisraeli hawakuweza kuangalia uso wake ingawa kungaa kule kulikuwa kwa muda tu.
8
Basi si zaidi sana matokeo ya utumishi wa Roho yatakuwa yenye utukufu?
9
Ikiwa utumishi unaowaletea watu hukumu ulikuwa na utukufu, basi si zaidi sana utumishi unaowafanya watu wahesabiwe haki mbele ya Mungu, utakuwa na utukufu mukubwa zaidi?
10
Tunaweza kusema kwamba ule utukufu uliongaa zamani hauwezi kulinganishwa na utukufu wa sasa unaokuwa mukubwa zaidi.
11
Kwa maana kama mambo yaliyokuwa ya muda tu yalipata utukufu, basi yale yanayodumu ni yenye utukufu zaidi.
12
Na kwa sababu tunakuwa na tumaini lile, sisi tunasema kwa uhodari.
13
Sisi hatufanyi kama Musa alivyokuwa akifunika uso wake na kitambaa kwa kuzuiza Waisraeli wasiangalie mwisho wa utukufu uliokuwa wa muda tu.
14
Lakini akili yao ilikuwa nzito kwa kufahamu. Kwa maana mpaka sasa, Waisraeli wanaposoma katika vitabu vya Agano la Kale, akili yao inafunikwa na kitambaa kile kile. Kitambaa kile kitaondolewa tu kwa mutu anayeungana na Kristo.
15
Mpaka sasa, kila mara wanaposoma katika vitabu vya Musa, kitambaa kinafunika akili yao.
16
Lakini “Wakati mutu anapomurudilia Bwana, kitambaa kile kinaondolewa.”
17
Hapa “Bwana” ni Roho; na pahali Roho wa Bwana anapokaa, pale kuna uhuru.
18
Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 4 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13