bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Samuel 21
2 Samuel 21
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 20
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 22 →
1
Wakati mumoja katika siku za utawala wa Daudi kukatokea njaa kali katika inchi. Njaa hiyo ilidumu miaka mitatu yenye kufuatana. Daudi alimwomba Yawe shauri. Yawe akamwambia: “Saulo na jamaa yake wana makosa ya kumwanga damu kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
2
Kwa hiyo, mufalme Daudi akawaita Wagibeoni. Wagibeoni hawakukuwa Waisraeli lakini walikuwa mabaki ya Waamori. Watu wa Israeli walikuwa wameapa kuwaacha wazima, lakini Saulo alijaribu kuwaua wote maana alikuwa na bidii ya upendeleo kwa watu wa Israeli na wa Yuda.
3
Daudi akawauliza Wagibeoni: “Niwatendee nini? Nitalipa namna gani maovu muliyotendewa kusudi mupate kuibariki inchi hii na watu wa Yawe?”
4
Wagibeoni wakamwambia: “Maneno kati yetu na Saulo pamoja na jamaa yake si jambo la kulipwa feza au zahabu, wala si jambo la kuua mutu yeyote katika inchi ya Israeli.” Mufalme akawauliza tena: “Sasa munasema niwatendee nini?”
5
Wao wakamwambia mufalme: “Saulo alikusudia kutuua sisi na kutuangamiza kusipate kubakia mutu yeyote wetu popote katika eneo lolote la Israeli.
6
Basi, utupatie watu saba kati ya wazao wake, nasi tuwatundike mbele ya Yawe juu ya mulima Gibea, kwa Saulo aliyechaguliwa na Yawe.” Mufalme akasema: “Nitawapatia nao.”
7
Mufalme alimwacha Mefiboseti mwana wa Yonatani kwa sababu ya kiapo ambacho Daudi na Yonatani mwana wa Saulo walikuwa wamefanya kati yao kwa jina la Yawe.
8
Lakini mufalme aliwatwaa wana wawili ambao Risipa binti ya Ahiya alimuzalia Saulo, nao ni: Armoni na Mefiboseti. Aliwatwaa vilevile watoto wote watano wanaume wa Mikali binti ya Saulo ambao alimuzalia Adrieli mwana wa Barzilayi wa muji Mehola.
9
Daudi aliwatoa watoto hao saba wanaume kwa Wagibeoni, nao wakawatundika kwenye mulima mbele ya Yawe, wote saba wakakufa pamoja. Watoto hao waliuawa kwa mwanzo wa mavuno ya Shayiri.
10
Kisha, Risipa binti ya Aya alitwaa nguo ya gunia, akajitandikia juu ya jiwe kubwa. Alikaa pale tangu mwanzo wa mavuno mpaka wakati wa mvua ulipofika na kuinyeshea maiti. Wakati huo wote, aliwafukuza ndege na wanyama wa pori, usiku na muchana, kusudi wasifikie maiti hizo.
11
Daudi alisikia yale Risipa binti ya Aya, habara ya Saulo aliyofanya.
12
Alikwenda na kuitwaa mifupa ya Saulo na ya mwana wake Yonatani kutoka kwa wakaaji wa Yabeshi-Gileadi, waliokuwa wameiiba kutoka kule Beti-Sani, ambako Wafilistini walikuwa wamemutundika Saulo na Yonatani siku ile walipomwua Saulo kwenye mulima Gilboa.
13
Daudi akairudisha mifupa ya Saulo na ya mwana wake Yonatani kutoka kule; na kisha wakakusanya mifupa ya vijana saba waliotundikwa.
14
Basi, watu wa Daudi wakaizika mifupa ya Saulo na ya mwana wake Yonatani katika inchi ya Benjamina, kule Zela katika kaburi la Kisi baba ya Saulo. Walifanya kila kitu ambacho mufalme aliamuru. Nyuma ya hayo, Yawe akayakubali maombi kwa ajili ya inchi.
15
Kisha Wafilistini walifanya vita tena na Waisraeli. Daudi na watu wake wakaenda kupigana na Wafilistini. Daudi alichoka sana siku ile.
16
Isibi-Benobi, mutu mumoja wa wazao wa majitu ambaye mukuki wake wa shaba ulikuwa na uzito wa karibu kilo tatu na nusu na aliyekuwa amejifungia upanga mupya, alisema atamwua Daudi.
17
Lakini Abisayi mwana wa Zeruya alikwenda kumusaidia Daudi. Abisayi alimushambulia yule Mufilistini na kumwua. Kwa hiyo, watu wakamwapia Daudi wakisema: “Hautakwenda tena nasi katika vita, kusudi usiizime taa ya ufalme katika Israeli.”
18
Nyuma ya hayo, kulitokea tena mapigano na Wafilistini kule Gobu. Kule, Sibekayi wa muji wa Husa alimwua Safu aliyekuwa mutu mumoja wa wazao wa Rafa.
19
Kulitokea tena mapigano na Wafilistini kule Gobu. Elihanani mwana wa Yare-Oregimu, wa muji wa Betelehemu, alimwua Goliati wa muji wa Gati, ambaye mupini wa mukuki wake ulikuwa kama muti wa mufumaji wa nguo.
20
Kisha kulitokea tena vita kule Gati ambako kulikuwa na mutu mumoja alikuwa murefu sana, na mwenye vidole sita katika kila mukono, na vidole sita katika kila muguu, jumla ya vidole vyake ilikuwa makumi mbili na ine. Yeye vilevile alikuwa wa uzao wa majitu.
21
Alipowachekelea Waisraeli, Yonatani mwana wa Simei, ndugu ya Daudi, alimwua.
22
Hao wane walikuwa wazao wa majitu kule Gati, nao waliuawa na Daudi pamoja na watumishi wake.
← Chapter 20
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 22 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24