bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 10
Deuteronomy 10
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 9
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 11 →
1
“Kisha Yawe akaniambia: ‘Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, na sanduku la mbao. Kuja kwangu huku juu kwenye mulima,
2
nami nitaandika maneno yaliyokuwa yameandikwa katika vibao vile ulivyovunja, kisha uweke vibao hivyo katika sanduku’.
3
“Basi, nikatengeneza sanduku la mushita na vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nikavitwaa katika mukono, nikapanda navyo kwenye mulima.
4
Yawe akaandika katika vibao hivyo maneno kama yaleyale ya kwanza: amri kumi ambazo aliwapa aliposema kutoka katika moto siku ya mukutano. Halafu Yawe akanipa vibao hivyo.
5
Nikageuka, nikashuka kutoka kwenye mulima, nikaweka vibao hivyo ndani ya sanduku nililokuwa nimetengeneza, na vimo ndani ya sanduku hilo, kama vile Yawe alivyoniamuru.”
6
(Watu wa Israeli wakasafiri kutoka visima vya watu wa Yakani mpaka Musara. Haruni akakufa na kuzikwa kule. Eleazari mwana wake, akatwaa nafasi yake kama vile kuhani.
7
Kutoka pale, wakasafiri mpaka Gudigoda, na kutoka Gudigoda mpaka Yotibata, eneo lenye vijito vingi vya maji.
8
Wakati huo, Yawe akachagua watu wa kabila la Lawi wakuwe wanabeba Sanduku la Agano la Yawe, wamutumikie kama vile makuhani na kubariki watu kwa jina lake hata hivi leo.
9
Ndiyo maana kabila la watu wa Lawi halina sehemu ya inchi ya urizi pamoja na wandugu zao. Walichopokea ni heshima ya kuwa makuhani wa Yawe, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyoahidi.)
10
“Nikakaa kwenye mulima kwa muda wa siku makumi ine, usiku na muchana, kama vile mbele. Yawe akanisikiliza kwa mara ingine tena na akakubali kutowaangamiza.
11
Kisha akaniambia: ‘Ondoka uendelee na safari yako ukiwaongoza watu kusudi waweze kuingia na kurizi inchi niliyowaapia babu zenu kwamba nitawapa’.
12
“Sasa, enyi Waisraeli, Yawe, Mungu wenu, anataka nini kwenu? Yawe, Mungu wenu, anataka mumwogope, mufuate njia zake zote, mumupende, mumutumikie Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wote na kwa roho yenu yote,
13
na mutii amri na masharti ya Yawe ninayowawekea leo, kwa mafaa yenu wenyewe.
14
Angalia, mbingu hata mbingu za mbingu ni mali ya Yawe, Mungu wenu, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake.
15
Tena Yawe alifurahia babu zenu kwa kuwapenda na akawachagua ninyi wazao wao pahali pa watu wengine wote, kama hivi leo.
16
Kwa hiyo, mutahiri magovi ya mioyo yenu, musikuwe wagumu tena.
17
Maana Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu wa miungu na Bwana wa wabwana. Yeye ni Mungu mukubwa na mwenye nguvu, na wa kuogopesha. Hapendelei wala hapokei kituliro.
18
Anatetea haki ya wayatima na wajane; vilevile anawapenda wageni na kuwapa chakula na nguo.
19
Basi, muwapende wageni kwa sababu nanyi vilevile mulikuwa wageni katika inchi ya Misri.
20
Mumwogope Yawe, Mungu wenu, mumutumikie, muambatane naye na kuapa kwa jina lake.
21
Yeye ni utukufu wenu. Yeye ni Mungu wenu ambaye amewatendea haya mambo makubwa na ya kutisha muliyoona kwa macho yenu wenyewe.
22
Babu zenu walipokwenda Misri, walikuwa watu makumi saba tu, lakini sasa Yawe, Mungu wenu, amewafanya kuwa wengi kama nyota mbinguni.
← Chapter 9
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 11 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34