bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 12
Deuteronomy 12
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 13 →
1
“Haya ndiyo masharti na maagizo ambayo mutatimiza katika inchi ambayo Yawe, Mungu wa babu zenu amewapa kwa kuirizi, siku zote za kuishi kwenu juu ya inchi.
2
Muharibu kabisa pahali pote ambapo watu wanaabudia miungu yao kwenye milima mirefu, vilima na chini ya miti yenye majani mabichi.
3
Muvunje mazabahu zao, na kubomoa kabisa nguzo zao. Muteketeze kwa moto sanamu zao za Ashera na kukatakata sanamu zao za kuchonga na kufuta kabisa jina lao na pahali hapo.
4
“Wala musimwabudu Yawe, Mungu wenu, namna hiyo yao.
5
Lakini mutakwenda pahali ambapo Yawe, Mungu wenu, atachagua katika makabila yote kwa kuweka jina lake na makao yake hapo. Huko ndiko mutakakokwenda.
6
Vilevile huko mutapeleka sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, matoleo yenu ya mapenzi na ya kutimiza kiapo, na wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu.
7
Huko, mutakula mbele ya Yawe, Mungu wenu, na mutafurahi ninyi pamoja na watu wa nyumba zenu kwa ajili ya mafanikio yenu Yawe, Mungu wenu, aliyowabarikia.
8
“Musifanye kama vile tunavyofanya sasa, kila mutu kama vile anavyopenda mwenyewe;
9
kwa sababu bado hamujaingia pahali pa kupumzikia na katika urizi Yawe, Mungu wenu, anaowapa.
10
Lakini mutakapovuka muto Yordani na kuishi katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapatia muirizi, na atakapowapatia pumziko musisumbuliwe na waadui zenu wote watakaowazunguka kusudi mupate kuishi salama,
11
basi huko pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kusudi jina lake likae pale, hapo mutapeleka yote ninayowaamuru: sadaka zenu za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, na sadaka za kutimiza kiapo.
12
Huko mutafurahi mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi kati yenu kwa sababu hawana sehemu wala urizi kati yenu.
13
Mufanye angalisho musitoe sadaka zenu za kuteketezwa pahali popote munapoona;
14
lakini pahali ambapo Yawe atakapopachagua katika kabila moja kati ya makabila yenu, hapo ndipo pahali mutakapotolea sadaka zenu za kuteketezwa na ni hapo mutakapofanyia mambo mengine yote ambayo nimewaamuru mufanye.
15
“Lakini muna uhuru wa kuchinja na kula nyama wenu popote katika makao yenu munavyopenda, kama vile baraka za Yawe, Mungu wenu, alizowapa, kadiri mutakavyojaliwa na Yawe. Watu wote, wanaokuwa safi au wachafu wanaweza kula, kama vile munavyokula nyama ya paa au ya kulungu.
16
Lakini musikule damu ya nyama hao; mumwange damu hiyo chini kama vile maji.
17
Musikule vitu hivi pahali munapoishi: sehemu ya kumi za ngano zenu, divai zenu au mafuta yenu, wazaliwa wa kwanza wa ngombe wenu au kondoo wenu, au sadaka zenu za kutimiza kiapo au za mapenzi, au matoleo mengine.
18
Mutavikula mbele ya Yawe, Mungu wenu, pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua. Mutavikula ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi katika miji yenu.
19
Vilevile muhakikishe kwamba hamutawasahau Walawi muda wote mutakaoishi katika inchi yenu.
20
“Yawe, Mungu wenu atakapopanua inchi yenu, kama vile alivyoahidi, nanyi mutasema: ‘Tutakula nyama’ kwa sababu munapenda nyama, munaweza kula nyama kiasi munachotaka.
21
Basi, pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua, apaweke jina lake, hapo munaweza kuchinja ngombe au kondoo yeyote ambaye Yawe amewajalia, kama nilivyowaamuru na munaweza kula kiasi chochote munachotaka cha nyama hiyo, kama mukiwa katika miji yenu.
22
Mutaikula nyama hiyo kama vile wanavyokula paa au kulungu. Mutu yeyote anaweza kula, anayekuwa safi na asiyekuwa safi.
23
Lakini muhakikishe kwamba hamukuli damu, maana damu ni uzima. Hivyo basi, musikule uzima pamoja na nyama.
24
Musikule damu hiyo, lakini muimwange chini kama vile maji.
25
Musikule damu, nanyi mutafanikiwa pamoja na wazao wenu, maana mutakuwa munatenda kwa usawa mbele ya Yawe.
26
Vitu vitakatifu mutakavyotoa na sadaka zenu za kutimiza kiapo, mutavitwaa na kuvipeleka pahali Yawe atakapochagua.
27
Hapo, mutatoa sadaka za kuteketezwa, nyama na damu, kwenye mazabahu ya Yawe, Mungu wenu. Damu ya nyama mutainyunyiza kwenye mazabahu ya Yawe Mungu wenu, lakini munaruhusiwa kula nyama.
28
Mufanye angalisho kutii maneno haya niliyowaamuru, kusudi mupate kufanikiwa ninyi pamoja na wazao wenu nyuma yenu milele, maana mutakuwa munatenda mazuri na kwa usawa mbele ya Yawe, Mungu wenu.
29
“Yawe, Mungu wenu ataangamiza mataifa mbele yenu, hayo ambayo munakwenda kuyafukuza, kuyatoa na kukaa katika inchi yao.
30
Atakapokwisha kuyaangamiza mbele yenu, mufanye angalisho musijiingize katika mutego kwa kuyafuata. Musijisumbue kujua kitu juu ya miungu yao, mukisema: ‘Mataifa haya yaliabudu namna gani miungu yake kusudi nasi tuwaabudu vile vile?’
31
Musimwabudu Yawe, Mungu wenu, hivyo, kwa maana kila chukizo ambalo Yawe hapendi, wameifanyia miungu yao, hata wamewachoma ndani ya moto watoto wao wanaume na wanawake, kwa kutambikia miungu yao.
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 13 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34