bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 13
Deuteronomy 13
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 12
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 14 →
1
“Kila kitu ambacho nimewaamuru, mufanye angalisho mukitende; musiongeze kitu wala musipunguze kitu.
2
“Kukitokea nabii au mutabiri wa kutumia ndoto kati yenu na kuwapatia kitambulisho au ajabu fulani,
3
kisha neno, vitambulisho au maajabu aliyowaambia yakitokea, na akisema: ‘Tufuate miungu mingine, miungu ambayo hamujapata kuijua, na tuitumikie’,
4
musisikilize maneno ya nabii huyo au mutabiri wa kutumia ndoto, kwa maana Yawe, Mungu wenu, anawatumia kwa kuwajaribu kusudi ajue kama munamupenda yeye Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.
5
Mufuate na kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kushika amri zake na kutii sauti yake. Mumutumikie na kuambatana naye.
6
Lakini nabii huyo au mutabiri wa kutumia ndoto atauawa, kwa sababu atakuwa amewafundisha uasi mbele ya Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa katika inchi ya Misri na kuwakomboa kutoka katika utumwa, kusudi muache njia ambayo Yawe, Mungu wenu, aliwaamuru kufuata. Hivi ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.
7
“Ikiwa ndugu yako wa tumbo moja, au mwana wako, au binti wako, au muke wako unayemupenda sana au rafiki yako mupenzi, atakushawishi kwa siri akisema: ‘Twende tuabudu miungu mingine’, ambayo wewe wala babu zenu hamwijui,
8
miungu ya watu wanaoishi karibu nanyi au miungu ya watu wanaoishi mbali tokea incha moja ya dunia mpaka incha nyingine,
9
usikubali kushawishiwa wala kumusikiliza, au kumuhurumia wala usimwachilie wala usimufiche;
10
lakini utamwua. Mukono wako unapaswa ukuwe wa kwanza wakati wa kumwua halafu wengine wote watafuata vilevile.
11
Umupige mawe mpaka akufe, kwa sababu amejaribu kukuvuta mbali kutoka kwa Yawe, Mungu wako, ambaye alikutoa toka utumwa katika inchi ya Misri.
12
Hivyo, Waisraeli wote watasikia na kuogopa, na hawatafanya uovu kama huo hata kidogo.
13
“Mutakapoishi katika miji ambayo Yawe, Mungu wenu anawapa, labda mutasikia
14
kwamba watu fulani wa ovyo ovyo kati yenu, wamewashawishi watu wa muji wakisema: ‘Twende tuabudu miungu mingine’, ambayo bado hamukujua,
15
basi mutapeleleza na kufanya uchunguzi na kuuliza kwa uangalifu. Na kama ni kweli kwamba jambo la kuchukiza limetendeka kati yenu,
16
hakika mutawaua kwa upanga watu wa muji huo. Mutauteketeza kwa upanga kabisa na ngombe wote vilevile.
17
Mutakusanya vitu vyote mulivyoteka katika kiwanja cha muji na kuchoma kwa moto vitu vile vyote kama vile sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yawe, Mungu wenu. Muji huo utakuwa lundo la mabomoko milele, nao hautajengwa tena.
18
Kitu ambacho kimekwisha kutolewa kiteketezwe musikitwae, kusudi Yawe aache ile hasira yake mbaya. Yawe, Mungu wenu, atawaonyesha rehema na kuwafanya ninyi mukuwe wengi sana kama vile alivyoahidia babu zenu,
19
kama tu mutatii sauti yake, mukishika amri zake zote ambazo ninawapa hivi leo na kufanya kile kinachokuwa sawa mbele yake.
← Chapter 12
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 14 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34