bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 14
Deuteronomy 14
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 13
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 15 →
1
“Ninyi ni watoto wa Yawe, Mungu wenu; musijichanje wala kunyoa nywele upande wa mbele kwa ajili ya mutu aliyekufa.
2
Ninyi ni watakatifu wa Yawe, Mungu wenu. Yawe amewachagua ninyi kuwa watu wake kati ya watu wote katika dunia yote.
3
“Musikule kitu kinachokuwa chukizo kwa Mungu.
4
Munaweza kula nyama hawa: ngombe, kondoo, mbuzi,
5
kulungu, paa, kongoni, mbuzi wa pori, paa mweupe, pofu na mbuzi wa mulima,
6
na kila nyama mwenye kwato zinazogawanyika sehemu mbili na mwenye kucheua.
7
Lakini musikule nyama yeyote ambaye kwato zake hazigawanyiki sehemu mbili na hacheui. Musikule ngamia, sungura na pelele, ingawa wanacheua lakini kwato zao hazigawanyiki sehemu mbili; hao ni wachafu kwenu.
8
Vilevile musikule nguruwe, maana ijapokuwa kwato zake zinagawanyika sehemu mbili, yeye hacheui; hao ni wachafu kwenu. Musikule nyama zao wala musiguse mizoga yao.
9
“Munaweza kula kila aina ya samaki wenye mapezi na magamba.
10
Lakini kiumbe chochote kinachoishi ndani ya maji kisichokuwa na mapezi wala magamba musikule; hivyo ni vichafu kwenu.
11
“Munaweza kula ndege wote wanaokuwa safi.
12
Lakini musikule ndege hawa: furukombe, kipungu,
13
kengewa, kozi, mwewe na aina zake,
14
kibombobombo na aina zake,
15
mbuni, kirukanjia, dudumizi, kipanga na aina zake,
16
bundi, mumbi, bundi mukubwa,
17
mwari, nderi, munandi,
18
membe, koikoi na aina zake, hudihudi na popo.
19
Na wadudu wote wenye mabawa ni wachafu kwenu; musiwakule.
20
Munaweza kula viumbe vyote vyenye mabawa vinavyokuwa safi.
21
Musikule nyamafu yeyote lakini munaweza kumupa mugeni anayeishi katika miji yenu, akule, au munaweza kumwuzishia mutu wa taifa lingine. Musipike mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake. “Ninyi ni watakatifu na Yawe ni Mungu wenu.
22
“Mutoe sehemu ya kumi ya mazao yenu yote ya shamba kila mwaka.
23
Halafu muende pahali ambapo Yawe, Mungu wenu amepachagua kwa kuweka jina lake, na mukiwa mbele yake mutakula sehemu ya kumi ya ngano yenu, ya divai yenu na ya mafuta, na ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu. Mufanye hivi kusudi mujifunze kumwogopa Yawe, Mungu wenu siku zote.
24
Ikiwa safari ni ndefu kwa sababu Yawe, Mungu wenu, amechagua pahali pa kuweka jina lake ambapo ni mbali sana na nyumba, nanyi hamuwezi kubeba sehemu ya kumi za mazao yenu ambayo Yawe amewajalia kupata, basi, mufanye hivi:
25
“Muuzishe mazao yenu na kupeleka feza hiyo mpaka pahali Yawe, Mungu wenu, alipochagua,
26
muzitumie hizo feza kwa kitu chochote mutakachopenda - nyama ya ngombe, nyama ya kondoo, divai au kinywaji kikali. Mutavikula na kufurahi hapo mbele ya Yawe, Mungu wenu, pamoja na jamaa zenu.
27
“Musiwasahau Walawi wanaoishi kati yenu; wao hawana fungu wala urizi wao kati yenu.
28
Kila mwisho wa mwaka wa tatu mutoe sehemu ya kumi ya mazao yenu yote na kuyaweka akiba katika miji yenu.
29
Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.
← Chapter 13
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 15 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34