bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 16
Deuteronomy 16
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 15
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 17 →
1
“Mushike mwezi wa Abibu na kufanya Pasaka kwa heshima ya Yawe, Mungu wenu. Maana katika mwezi huo wa Abibu, Yawe, Mungu wenu aliwatoa Misri wakati wa usiku.
2
Mutatoa sadaka ya Pasaka kutoka mifugo yenu ya kondoo au ngombe kwa heshima ya Yawe pahali ambapo Yawe atachagua kwa ajili ya jina lake.
3
Musikule sadaka hiyo na mikate iliyotiwa chachu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso – kwa sababu mulitoka Misri kwa haraka; kwa hiyo, muda wote mutakaoishi mutakumbuka ile siku mulipotoka Misri.
4
Kwa muda wa siku saba mutu yeyote katika inchi yenu asiweke chachu ndani ya nyumba yake, na nyama ya yule nyama aliyechinjwa magaribi ya siku ya kwanza isibaki mpaka asubui.
5
Musitolee sadaka ya Pasaka katika muji wowote ambao Yawe, Mungu wenu, atawapa;
6
lakini mutaitolea pale pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kwa ajili ya jina lake. Mutatolea sadaka ya Pasaka magaribi, jua linapotua, wakati uleule mulipotoka Misri.
7
Hiyo nyama mutaipika na kuikula pahali pale Yawe, Mungu wenu atakapochagua. Asubui yake mutageuka na kurudi katika mahema zenu.
8
Katika siku sita mutakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya saba kutakuwa mukutano mukubwa wa kumwabudu Yawe, na hamutafanya kazi yoyote katika siku hiyo.
9
“Mutahesabu majuma saba; mutaanza kuyahesabu tangu munapoanza kuvuna ngano.
10
Halafu mutafanya sikukuu ya majuma kwa heshima ya Yawe, Mungu wenu, kwa kutoa sadaka ya mapenzi kadiri Yawe, Mungu wenu, anavyowabariki.
11
Mutafurahia mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi pamoja nanyi. Mufanye haya katika pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kwa ajili ya jina lake.
12
Mukumbuke kwamba mulikuwa watumwa kule Misri na mukuwe waangalifu kufuata masharti haya.
13
“Kisha kupepeta ngano yenu yote na kukamua zabibu zenu, mutafanya sikukuu ya vibanda kwa muda wa siku saba.
14
Mutafanya karamu hiyo, ninyi na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.
15
Kwa siku saba mutamufanyia Yawe, Mungu wenu, karamu pahali ambapo Yawe atachagua; kwa sababu Yawe, Mungu wenu atawabariki kwa mazao yenu yote na katika shuguli zenu zote nanyi hakika mutafurahi.
16
“Wanaume wote wa taifa lenu watakuja mbele ya Yawe, Mungu wenu, mara tatu kila mwaka, pahali ambapo Yawe, Mungu wenu atachagua: wakati wa sikukuu ya Pasaka, sikukuu ya kuvuna na wakati wa sikukuu ya vibanda. Wasitokee mbele ya Yawe mikono mitupu.
17
Wote watatoa kadiri wanavyoweza kulingana na baraka Yawe, Mungu wenu, alizowajalia.
18
“Mutachagua waamuzi na wakubwa kutoka makabila yenu katika miji yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapa nao watatoa hukumu za haki kwa watu.
19
Musipotoshe haki, musikuwe na upendeleo, wala musikubali kupokea kituliro, kwa kuwa kituliro kinapofusha macho ya watu wenye hekima na kupotosha maneno ya mutu mwenye haki.
20
Mutafuata yanayokuwa ya haki tu, kusudi mupate kuishi na kurizi inchi munayopewa na Yawe, Mungu wenu.
21
“Musipande muti wowote ukuwe nguzo ya mungu wa uongo karibu na mazabahu mutakayomujengea Yawe, Mungu wenu.
22
Wala musisimamishe nguzo ambayo Yawe Mungu wenu anaichukia.
← Chapter 15
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 17 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34