bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 17
Deuteronomy 17
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 16
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 18 →
1
“Musitoe sadaka kwa Yawe, Mungu wenu, ngombe au kondoo mwenye kilema; hiyo ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu.
2
“Kama mukisikia katika mumoja wa miji yenu kuna mwanaume au mwanamuke anayetenda maovu mbele ya Yawe, Mungu wenu, na kuvunja agano lake
3
naye amekwenda na kutumikia miungu mingine na kuiabudu, akiabudu jua, mwezi au vitu vingine vya mbinguni nisivyoagiza,
4
mutafanya uchunguzi kamili, na kama ni kweli kwamba kitu hiki kiovu kimefanywa katika Israeli,
5
basi, mumupeleke mutu huyo inje ya miji na kumupiga mawe mpaka akufe.
6
Hata hivyo, atauawa ikiwa kuna ushuhuda wa watu wawili au watatu. Asiuawe ikiwa kuna ushuhuda wa mutu mumoja tu.
7
Wale washuhuda ndio watakaoanza kumupiga mawe kwanza, halafu wengine wamupige mawe. Ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.
8
Inawezekana kutatokea mashitaki mengine yanayokuwa magumu ndani ya miji yenu, kama vile maneno yanayoelekea uchafu, mambo ya haki za watu, na hasara ya mwili. Basi, mutaondoka na kwenda pahali Yawe, Mungu wenu alipopachagua,
9
na huko mutawaendea makuhani wa Kilawi, na mwamuzi ambaye yuko katika kazi kwa wakati huo, nanyi mutatoa mashitaki kwao nao watawatangazia uamuzi wao.
10
Kisha mutafanya kama vile watakavyowatangazia pale pahali Yawe atakapochagua. Mutakuwa waangalifu kufanya yote kama vile watakavyowaagiza.
11
Itawapasa kufanya kufuatana na maongozi watakayowapatia na uamuzi watakaotoa kwenu. Musiache kutimiza hukumu watakayowatangazia kwa kupita kuume au kushoto.
12
Naye mutu atakayetenda kwa kiburi bila kutii kuhani aliyewekwa hapo kwa kumutumikia Yawe, Mungu wenu, au mwamuzi, mutu huyo atauawa. Ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.
13
Watu wote watasikia na kuogopa wasifanye tena kitu kwa kiburi.
14
“Mutakapokwisha kuingia katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa, mukirizi na kukaa humo, nanyi mukisema kwamba mutaweka mufalme juu yenu, kama vile mataifa yote yanayowazunguka,
15
munaweza kumuweka mufalme juu yenu mutu ambaye Yawe, Mungu wenu, atamuchagua. Mutamuweka mumoja wa wandugu zenu kuwa mufalme juu yenu. Musimufanye mugeni asiyekuwa ndugu yenu kuwa mufalme wenu.
16
Hata hivyo, asikuwe na farasi wengi kwa ajili yake mwenyewe, wala asiwarudishe watu Misri kwa kujipatia farasi zaidi, kwa sababu Yawe amewaonya: ‘Hamutarudi tena kwa njia ile.’
17
Wala asijipatie wake wengi; kama sivyo moyo wake utaasi. Wala asijipatie feza na zahabu kwa wingi sana.
18
Atakapokuwa akiikalia kiti cha ufalme anapaswa kuandika mufano wa sheria hii katika kitabu kinachokuwa mbele ya makuhani wa Kilawi.
19
Mufano huo atakuwa nao siku zote na kuusoma maisha yake yote, kusudi apate kujifunza kumwogopa Yawe, Mungu wake, akishika na kutimiza maneno yote ya sheria hii na masharti haya,
20
bila kujitukuza mwenyewe juu ya wandugu zake, wala kuiweka kando amri hii kwa namna yoyote, kusudi aweze kudumu katika utawala, yeye na wazao wake katika Israeli.
← Chapter 16
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 18 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34