bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 18
Deuteronomy 18
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 17
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 19 →
1
“Makuhani Walawi, ni kusema kabila lote la Lawi, wasikuwe na sehemu wala urizi katika Israeli. Wao watakula sehemu ya sadaka za Yawe.
2
Wala wasikuwe na urizi kati ya wandugu zao; Yawe ndiye urizi wao kama vile alivyoahidi.
3
“Na hii itakuwa haki ya makuhani kutoka kwa watu wanaotolea sadaka ikuwe ni ngombe au kondoo: watamupa kuhani muguu wa mbele, mashavu na matumbotumbo.
4
Mutawapa sehemu ya kwanza ya mazao yenu ya ngano, divai, mafuta yenu na sufu ya kwanza ya kondoo wenu.
5
Katika makabila yenu yote, Yawe amechagua kabila la Walawi limutumikie kama vile makuhani milele.
6
“Ikiwa Mulawi yeyote atapenda mwenyewe anaweza kutoka katika muji wowote wa Israeli kwenda pale pahali Yawe alipochagua,
7
na hapo anaweza kutumika kwa jina la Yawe, Mungu wake, kama wale Walawi wengine wanaotumika mbele ya Yawe.
8
Watapata mafungu yao sawa ya kula, ingawa wako na mapato kutokana na kuuzisha mali za jamaa zao.
9
“Mutakapofika katika ile inchi Yawe, Mungu wenu, anayowapa, musifuate zile tabia za kuchukiza za mataifa ya huko.
10
Kusikuwe mutu yeyote kati yenu anayemupitisha kwenye moto mutoto wake mwanaume au mwanamuke kuwa tambiko, wala mutu anayepiga ramuli, wala mwaguzi, wala mwenye kufanya uganga,
11
wala muchawi, wala mulozi, wala mwenye kutaka shauri kwa mizimu na pepo au kutoka kwa wafu.
12
Maana yeyote anayetenda mambo haya ni chukizo kwa Yawe; na kwa ajili ya mambo haya ya kuchukiza Yawe, Mungu wenu, anafukuza watu wa namna hiyo mbele yenu.
13
Mukuwe wakamilifu mbele ya Yawe, Mungu wenu.
14
Kwa maana mataifa haya ambayo mutairizi inchi yao wanafuata maongozi ya waaguzi na wapiga ramuli; lakini Yawe, Mungu wenu hawaruhusu ninyi kufanya hivyo.
15
“Yawe, Mungu wenu atawachagulia nabii anayekuwa kama mimi kutoka kati yenu wenyewe, nanyi mutamutii huyo.
16
Hicho ndicho mulichomwomba Yawe, Mungu wenu, kule Horebu, siku ile mulipokusanyika na kusema: ‘Tusisikie tena sauti ya Yawe, Mungu wetu, wala tusiuone tena moto huu mukubwa, kusudi tusikufe!’
17
Naye Yawe akaniambia: ‘Wamesema ukweli.
18
Nitawachagulia kati ya wandugu zao wenyewe nabii kama wewe, nitatia maneno yangu ndani ya kinywa chake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.
19
Yeyote ambaye hatasikia maneno nabii huyo atakayosema kwa jina langu, mimi mwenyewe nitamwazibu.
20
Lakini nabii yeyote atakayesema kwa jina la miungu mingine, au atakayejaribu kusema neno kwa jina langu wakati mimi sikumwambia aseme, huyo nabii atakufa.’
21
“Lakini ninyi munaweza kusema: ‘Tutaweza namna gani kutambua neno ambalo Yawe hakulisema?’
22
Kama nabii akisema kitu aseme ni kwa jina la Yawe, na kitu hicho hakifanyiki au hakiko kweli, jambo hilo Yawe hakulisema; nabii amelisema kwa kiburi, nanyi musitishwe na jambo hilo.
← Chapter 17
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 19 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34