bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 19
Deuteronomy 19
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 18
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 20 →
1
“Wakati Yawe, Mungu wenu, atakapoteketeza watu wale ambao anawapa ninyi inchi yao, na kisha kuitwaa na kuishi katika nyumba zao,
2
mutatenga miji mitatu katika inchi Yawe, Mungu wenu atakayowapatia muirizi.
3
Mutatengeneza barabara na kugawanya katika sehemu tatu inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapatia muirizi kusudi yeyote anayemwua mutu bila kukusudia apate kukimbilia huko.
4
“Mutu kwa bahati mbaya akimwua mwenzake bila kukusudia ambaye kwanza hakuwa adui yake,
5
kwa mufano, mutu anayekwenda na mwenzake katika pori kukata kuni naye wakati anakata muti, shoka likachomoka kutoka kwenye mupini wake, na kumwua yule mwingine, mutu huyo anaweza kukimbilia kwenye muji mumoja, kwa kuokoa maisha yake.
6
Lakini kama umbali wa muji huo ni mukubwa sana, huyo mwenye kulipiza kisasi, kwa hasira kali anaweza kumufuatilia, akimukamata na kumwua huyo aliyesababisha kifo, ingawa hakupewa hukumu ya kifo na hao wawili hawakukuwa waadui mbele.
7
Kwa hiyo mimi ninawaamuru mutenge miji mitatu.
8
“Tena kama vile Yawe, Mungu wenu, akipanua mipaka ya inchi yenu, kama vile alivyowaapia babu zenu, naye akiwapatia inchi yote ambayo aliahidi kuwapatia hao babu zenu
9
ikiwa mutakuwa waangalifu kushika amri hizi zote, ninazowaamuru hivi leo, mukimupenda Yawe, Mungu wenu, na kufuata siku zote njia zake, basi, mutaongeza miji mingine mitatu zaidi ya hii mitatu,
10
kusudi mutu asiyekuwa na kosa asiuawe katika inchi yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapatia kuwa yenu, na hivyo kuwasababisha kuwa na kosa la mauaji.
11
“Lakini mutu akiwa adui wa mwenzake, akivizia, akimushambulia na kumwua, kisha anakimbilia kwenye muji mumoja wa miji hiyo,
12
hapo wazee wa muji huo watatuma watu wamutoshe kule na kumutoa kwa mwenye kulipiza kisasi cha umwangaji wa damu, auawe.
13
Musimwonee huruma, lakini mutakomesha uovu wa mauaji ya mutu asiyekuwa na kosa katika Israeli, kusudi mupate kuishi kwa amani.
14
“Musiondoe kitambulisho cha mipaka ya wajirani zenu, ambayo iliwekwa hapo zamani katika inchi ambayo Yawe wenu anawapatia muirizi.
15
“Ushuhuda wa mutu mumoja hautoshi kwa kuhukumu mutu juu ya kosa lolote au uovu juu ya kosa lolote alilofanya. Ni ushuhuda wa watu wawili au watatu tu ndio utakaohakishwa.
16
Ikiwa mushuhuda wa uongo atatokea kwa kumushitaki mutu yeyote juu ya kosa fulani,
17
basi hao wote wawili wanaobishana watakwenda mbele ya Yawe, mbele ya makuhani na waamuzi ambao wako katika kazi wakati huo.
18
Waamuzi watachunguza kwa uangalifu maneno hayo na ikiwa mushuhuda ni mushuhuda wa uongo na amemushitaki mwenzake kwa uongo,
19
basi, mutamutendea sawa vile alivyokusudia kumutendea ndugu yake. Ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.
20
Nao watu wengine watasikia na kuogopa, na uovu kama huo hautafanyika tena kati yenu.
21
Musiwaonee huruma watu wa aina hiyo. Uzima utalipwa kwa uzima, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mukono kwa mukono na muguu kwa muguu.
← Chapter 18
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 20 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34