bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 20
Deuteronomy 20
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 19
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 21 →
1
“Mukienda kwa vita kupigana na waadui zenu, mukiona farasi, magari na jeshi kubwa zaidi kuliko lenu musiwaogope. Maana Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa Misri, atakuwa nanyi.
2
Mbele ya kuanza mapigano, kuhani atajitokeza mbele na kuwaambia watu:
3
‘Watu wa Israeli musikilize! Leo munakaribia kupigana na waadui zenu. Musivunjike moyo, au kuogopa, au kutishwa, au kuwaogopa waadui;
4
maana Yawe, Mungu wenu, ndiye atakayekwenda pamoja nanyi kupigana kwa ajili yenu mbele ya waadui zenu na kuwapa ushindi’.
5
“Kisha wakubwa watawaambia watu: ‘Kuna mutu yeyote hapa aliyejenga nyumba mupya lakini hajaizindua? Arudie kwake, kusudi asikufie kwenye vita na mutu mwingine aizindue.
6
Kuna mutu yeyote hapa aliyepanda mizabibu na ambaye hajafurahia matunda yake ya kwanza? Arudi kwake asikufie kwenye vita na mutu mwingine afurahie matunda yake.
7
Kuna mwanaume yeyote hapa aliyechumbia na yuko karibu kuoa? Arudie kwake, kusudi asikufie kwenye vita, na mwanaume mwingine aoe muchumba wake.
8
Kuna mutu aliyevunjika moyo? Arudie kwake, kusudi asiwavunje wenzake moyo kama vile yeye.’
9
Wakubwa wakisha kusema na watu, basi majemadari watawaongoza watu.
10
“Munapokaribia muji kwa kuushambulia, kwanza muwape wakaaji wake masharti ya amani.
11
Wakaaji wa muji huo wakitaka amani na kujitoa kwenu, basi watu wote wanaokuwa humo watawatumikia na kufanya kazi za kulazimishwa.
12
Lakini wakaaji wa muji huo wasipofanya amani nanyi, lakini wakipigana vita nanyi, basi, mutazunguka muji wao kwa vita,
13
naye Yawe, Mungu wenu, akiutia katika mikono yenu, mutawaua kwa upanga wanaume wote.
14
Lakini wanawake na watoto, ngombe, na vyote vinavyokuwa katika muji, vitu vyake vyote munaweza kuvibeba kwa ajili yenu wenyewe. Munaweza kufurahia vitu vya waadui zenu, ambavyo Yawe, Mungu wenu, amewapa.
15
Ndivyo mutakavyoitendea miji yote ambayo iko mbali na inchi mutakayorizi.
16
Lakini katika miji ya inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa, musiache kitu chochote.
17
Mutawaangamiza watu wote: Wahiti, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi na Wayebusi kama vile Yawe, Mungu wenu alivyoamuru,
18
kusudi wasiwafundishe desturi zao za kuchukiza ambazo wanafanyia miungu yao, nanyi mutende zambi mbele ya Yawe, Mungu wenu.
19
“Munapozunguka muji kwa muda murefu, mukipigana vita na kuuteka, musiharibu miti ya matunda kwa mashoka. Miti ni watu hata ishambuliwe nanyi? Munaweza kula matunda ya miti hiyo, lakini musiikate.
20
Munaweza kukata tu miti mingine kwa kuitumia kwa kujenga ngazi za kupandia ndani ya muji munaoshambulia mpaka uanguke.
← Chapter 19
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 21 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34