bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 21
Deuteronomy 21
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 20
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 22 →
1
“Mutu akipatikana ameuawa katika mbuga katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa kuwa urizi wenu, nanyi hamujui ni nani aliyemwua,
2
wazee na waamuzi wenu watajitokeza na kupima umbali wa kutoka pahali maiti inapokuwa mpaka kwenye miji ya karibu.
3
Kisha, wazee wa muji ule unaokuwa karibu zaidi na ile maiti watatwaa mwana-ngombe ambaye hajatumiwa kufanya kazi yoyote wala kutiwa nira.
4
Nao watamuteremusha mwana-ngombe katika bonde kwenye kijito ambacho hakikauki, na bonde hilo halilimwi au kupandwa. Huko watamuvunja huyo mwana-ngombe shingo.
5
Nao makuhani wa ukoo wa Lawi sharti wakuwe pale. Yawe, Mungu wenu, aliwachagua wamutumikie na kubariki kwa jina lake. Wao vilevile ndio wenye mamlaka ya kuamua magomvi na maneno juu ya kuumizana.
6
Yule mwana-ngombe atakapovunjwa shingo, wazee wote wa muji huo unaokuwa karibu na mutu huyo aliyeuawa, watanawa mikono yao kwa maji juu ya mwana-ngombe
7
na kusema: ‘Hatuna kosa juu ya kifo hiki, wala hatumujui aliyemwua.
8
Ee Yawe, uwasamehe watu wako wa Israeli ambao umewakomboa, usiwawekee watu wako Israeli kosa la mauaji ya mutu asiyekuwa na kosa, lakini uwasamehe kosa lile.’
9
Hivyo damu hiyo iliyomwangwa haitakuwa tena sababu ya hukumu kwenu, maana mumefanya yale Yawe aliyotaka mufanye.
10
“Mukienda kupigana vita na adui, naye Yawe akiwapa ushindi, na kuteka vitu,
11
kama mumoja wenu akiona kati ya vitu vilivyotekwa mwanamuke muzuri, akimutamani na kutaka kumwoa,
12
basi, anaweza kumupeleka kwake. Yule mwanamuke atanyoa kichwa chake na kukata kucha zake,
13
na kubadilisha nguo zake za kitumwa. Atakaa muda wa mwezi muzima kwa kumwomboleza baba yake na mama yake. Kisha mwanaume huyo anaweza kumwoa.
14
Kama kisha hapendezwi naye, atamwacha aende anakotaka. Mwanaume huyo hatamwuzisha kwa kupata feza, wala hatamutendea kama vile mutumwa kwa sababu amemunyenyekeza.
15
“Ikiwa mwanaume fulani ana wake wawili naye anamupenda mumoja kuliko mwingine, nao wanawake hao wamemuzalia watoto wanaume, na mutoto wa kwanza kuzaliwa ni wa yule mama asiyemupenda,
16
ikifika siku ya kuwapa hao wanawake urizi, huyo baba haruhusiwi kumutendea mutoto wa yule muke anayemupenda kama kwamba ni mutoto muzaliwa wa kwanza, pahali pa yule mutoto wa mama asiyependwa ambaye ndiye anayekuwa muzaliwa wa kwanza.
17
Anapaswa kukubali yule muzaliwa wa kwanza, mutoto wa yule mwanamuke asiyependwa, na kumupa haki yake: sehemu ya mali zake mara mbili.
18
“Kama mutu ana mutoto mwenye kiburi na mwasi, asiyemutii baba yake au mama yake ingawa wanamwazibu,
19
basi, mama na baba ya huyo mutoto watamutwaa kumupeleka kwa wazee muji kwenye tribinali.
20
Wazazi hao watawaambia wazee wa muji: ‘Mutoto wetu ni mwenye kiburi na mwasi, hataki kutusikiliza, ni mulafi na mulevi’.
21
Hapo watu wa muji huo watamupiga mutoto huyo mawe mpaka akufe. Ndivyo mutakavyokomesha ubaya huo kati yenu. Kila mutu katika Israeli atasikia tukio hilo na kuogopa.
22
“Kama mutu amefanya kosa linalomupasa auawe na akiuawa kwa kutundikwa juu ya muti,
23
maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.
← Chapter 20
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 22 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34