bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 23
Deuteronomy 23
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 22
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 24 →
1
“Mwanaume yeyote asilale na muke wa baba yake.
2
“Mwanaume yeyote aliyeumizwa au aliyekatwa kiungo chake cha kiume haruhusiwi kujiunga na kusanyiko la watu wa Yawe.
3
“Na mwana haramu yeyote, wala muzao wake hata kizazi cha kumi, haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe.
4
“Mwamori au Mumoabu yeyote, wazao wao wote hata kizazi cha kumi, hawaruhusiwi kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe,
5
kwa sababu walikataa kuwapatia chakula na maji mulipokuwa katika njia kutoka Misri, na kwa sababu walimulipa Balamu mwana wa Beori kutoka Petori kule Mesopotamia, awalaani.
6
Lakini Yawe, Mungu wenu, hakumusikiliza Balamu; pahali pake laana hiyo iligeuka kuwa baraka, kwa sababu Yawe, Mungu wenu, aliwapenda.
7
Kwa hiyo, musiwasaidie hao hata kidogo kusudi wapate amani na fanaka.
8
“Musiwachukie Waedomu; hao ni wandugu zenu. Na musiwachukie Wamisri, maana mulikaa katika inchi yao kama vile wageni.
9
Wazao wao, kuanzia kizazi cha tatu, wataruhusiwa kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe.
10
“Mukienda kwa vita, mukipiga kambi, kila mumoja afanye angalisho na kitu chochote kiovu.
11
Kama kati yenu kuna mutu yeyote ambaye ni muchafu kwa sababu ya kutokwa mbegu usiku, huyo atatoka inje ya kambi; hatakaa karibu na kambi.
12
Lakini ikifika magaribi ataoga, na jua likitua anaweza kurudi katika kambi.
13
“Munapaswa kuwa na pahali inje ya kambi ambapo munaweza kwenda kwa choo.
14
Kati ya vifaa vyenu mutakuwa na jembe, na hilo mutalitumia kuchimba shimo na kufukia mavi yenu.
15
Kambi yenu inapaswa kuwa takatifu kwa sababu Yawe, Mungu wenu anatembea katika kambi yenu kusudi awaokoe na kuwatia waadui zenu katika mikono yenu. Kwa hiyo musimwache aone kitu chochote kisichofaa kati yenu, kama sivyo atawaacha ninyi.
16
“Mutumwa akikimbilia kwako usimurudishe kwa bwana wake.
17
Ataishi pamoja nawe pahali atakapochagua katika moja ya makao yako, pahali panapomupendeza. Usimutese.
18
“Mwisraeli yeyote, mwanaume au mwanamuke, hatakuwa hata kidogo kahaba wa kidini.
19
Feza yoyote iliyopatikana na vitendo vya ukahaba huo, isipelekwe ndani ya hekalu la Yawe, Mungu wenu, kwa kulipia kiapo, maana mwanaume au mwanamuke anayekuwa kahaba wa kidini ni chukizo kwa Yawe.
20
“Usimukopeshe ndugu yako Mwisraeli kitu kwa faida; usimulipishe faida juu ya mukopo wa feza, chakula, au chochote ambacho watu wanakopesha kwa faida.
21
Unaweza kuomba faida unapomukopesha mugeni, lakini ndugu yako Mwisraeli usimulipishe faida, naye Yawe, Mungu wako, atakubariki katika shuguli zako zote utakazofanya katika inchi ambayo unakwenda kurizi.
22
Unapofanya kiapo mbele ya Yawe, Mungu wako, usichelewe kukitimiza, maana Yawe, Mungu wako, atakidai kwako, nawe utakuwa na kosa.
23
Lakini ukiacha kufanya kiapo hautakuwa na zambi.
24
Ukuwe mwangalifu kutimiza kiapo ulichosema kwa mudomo wako, maana ulimwahidi Yawe, Mungu wako, kwa mapenzi yako.
25
“Ukipitia katika shamba la muzabibu la mwenzako unaweza kula zabibu kadiri unavyoweza, lakini usichume na kupeleka zabibu zozote katika kikapu chako.
26
Ukipitia katika shamba la mwenzako lenye ngano unaweza kukwanyua masuke kwa mukono na kula, lakini usitwae kisu kwa kukata mazao yake.
← Chapter 22
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 24 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34