bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 27
Deuteronomy 27
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 26
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 28 →
1
Basi, Musa akiwa pamoja na wazee wa Israeli aliwaambia watu hivi: “Mushike amri zote ninazowapa leo.
2
Siku ile mutakapovuka muto Yordani na kuingia katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, amewapa, mutasimika mawe makubwa na kuyapiga lipu.
3
Juu yake mutaandika maneno yote ya sheria hizi zote, mutakapoingia katika inchi ile inayotiririka maziwa na asali, ambayo Yawe, Mungu wa wazee wenu, aliwaahidi.
4
Mukiwa ngambo ya muto Yordani, mutasimika mawe hata juu ya mulima Ebali, kama vile ninavyowaamuru hivi leo, na kuyapiga lipu.
5
Mutamujengea Yawe, Mungu wenu, mazabahu pahali pale panapokuwa na mawe ambayo hayakuchongwa.
6
Mutamujengea Yawe, Mungu wenu, mazabahu kwa mawe yasiyochongwa. Juu ya mazabahu hiyo mutamutolea Yawe, Mungu wenu, sadaka za kuteketezwa.
7
Mutamutolea sadaka za amani, na kula hapohapo na kufurahi mbele ya Yawe, Mungu wenu.
8
Mutaandika waziwazi juu ya mawe hayo maneno yote ya sheria hii.”
9
Basi, Musa pamoja na makuhani Walawi wakawaambia watu wote wa Israeli: “Munyamaze munisikilize enyi watu wa Israeli. Leo hii ninyi mumekuwa watu wa Yawe, Mungu wenu.
10
Kwa hiyo mutatii sauti ya Yawe, Mungu wenu, mukifuata amri zake na masharti yake ambayo ninawaamuru leo.”
11
Siku hiyo Musa akawaagiza watu na kusema:
12
“Mukisha kuvuka Yordani, makabila haya yatasimama juu na mulima Gerizimu kwa kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benjamina.
13
Na makabila haya yatasimama juu ya mulima Ebali wakati laana zitakapotolewa: Rubeni, Gadi, Aseri, Zebuluni, Dani na Nafutali.
14
Nao Walawi watatangazia watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
15
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayefanya sanamu ya kuchonga au ya kuyeyushwa na kuisimamisha kwa siri, kitu ambacho kimetengenezwa na mikono ya fundi na ambacho ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
16
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayezarau baba yake au mama yake.’ Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
17
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayeondoa kitambulisho cha mupaka wa mwenzake.’ Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
18
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayemupotosha kipofu katika njia.’ Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
19
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayepotosha haki ya mugeni au yatima au mujane’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
20
“ ‘Alaaniwe mwanaume anayelala na muke wa baba yake, maana amemupatisha baba yake haya’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
21
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayelala na nyama yoyote’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
22
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayelala na dada yake akuwe ni binti ya baba yake au binti ya mama yake’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
23
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayelala na mama mukwe wake’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
24
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayeua mutu kwa siri’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
25
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayepokea kituliro kusudi aue mutu asiyekuwa na kosa’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
26
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote asiyekubali maneno haya ya sheria na kuyatii’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
← Chapter 26
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 28 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34