bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 30
Deuteronomy 30
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 29
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 31 →
1
Musa akaendelea kusema: “Baraka na laana hizi zote zitatimizwa. Mutafikiri juu ya mambo hayo wakati Yawe, Mungu wenu, atakuwa amewatawanya kati ya mataifa.
2
Mukimurudilia Yawe, Mungu wenu, ninyi na watoto wenu, mukitii kwa moyo wote na roho yote neno lake ninalowaamuru leo,
3
hapo Yawe, Mungu wenu, atawarudishia mema yenu na kuwahurumia na kuwakusanya tena kutoka katika mataifa ambamo atakuwa amewatawanya.
4
Na hata kama mumetawanywa katika sehemu mbali kabisa katika dunia, Yawe, Mungu wenu, atawakusanya na kuwarudisha,
5
kwa kurizi tena inchi ambamo wazee wenu waliishi. Naye atawafanya mufanikiwe zaidi na kuwa wengi kuliko wazee wenu.
6
Yawe, Mungu wenu, atawafanya ninyi na wazao wenu mukuwe na moyo wa utii kusudi mumupende yeye kwa moyo wenu wote na roho yenu, mupate kuishi.
7
Yawe, Mungu wenu, atafanya laana hizi zote ziwapate waadui zenu ambao waliwatesa.
8
Nanyi mutatii sauti ya Yawe na kushika amri zake zote ninazowapa leo.
9
Yawe, Mungu wenu, atawafanya mufanikiwe katika kila mutakalofanya; mutakuwa na watoto wengi na ngombe wengi na mashamba yenu yatatoa mazao. Maana atapenda tena kuwafanya mufanikiwe kama vile alivyopenda kuwafanikisha wazee wenu,
10
ikiwa mutatii sauti yake na kushika amri na masharti yake yaliyoandikwa katika kitabu hiki cha sheria na kumurudilia Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wote na roho yote.
11
“Amri ninazowapa leo si ngumu sana kwenu, wala haziko mbali nanyi.
12
Haziko mbinguni hata museme: ‘Nani atakayepanda juu mbinguni kutuletea kusudi tupate kuzisikia na kuzitii?’
13
Wala haziko ngambo ya bahari, hata museme: ‘Nani atakayevuka bahari atuletee kusudi tuzisikie na kuzitii.’
14
Sivyo, lakini neno hili liko karibu nanyi, ndani ya vinywa vyenu na ndani ya mioyo yenu, mupate kulitimiza.
15
“Leo hii ninawapa uchaguzi kati ya mema na mabaya, kati ya uzima na kifo.
16
Kama mukitii amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa leo, mukimupenda Yawe, Mungu wenu, na kufuata njia zake na kushika amri, masharti na maagizo yake, basi, mutaishi na kuongezeka; naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika inchi ambayo munakwenda kuirizi.
17
Lakini mukipotoshwa na kukataa kumusikiliza, mukivutwa kuabudu miungu mingine na kuitumikia,
18
mimi ninawatangazia leo hii kwamba mutaangamia. Hamutaishi kwa muda murefu katika inchi munayokwenda kurizi, ngambo ya muto Yordani.
19
Ninaita mbingu na inchi zishuhudie juu yenu leo hii, kwamba nimewapa uchaguzi kati ya uzima na kifo, kati ya baraka na laana. Basi, muchague uzima ninyi na wazao wenu mupate kuishi.
20
Mumupende Yawe, Mungu wenu. Muitii sauti yake na kuambatana naye. Kama munafanya hivyo, mutapata maisha marefu na kuishi katika inchi ambayo Yawe aliwaahidi wazee wenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo, kwamba atawapa.”
← Chapter 29
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 31 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34