bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 33
Deuteronomy 33
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 32
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 34 →
1
Hii ndiyo baraka ambayo Musa, mutu wa Mungu aliwatakia Waisraeli mbele ya kufa kwake. Alisema hivi:
2
Yawe alikuja kutoka mulima Sinai, alitutokea kutoka mulima Seiri, aliangaza kutoka mulima Parani. Alitokea kati ya maelfu ya wamalaika, na moto unaowaka katika mukono wake wa kuume.
3
Yawe anawapenda watu wake, anawalinda watakatifu wake wote. Wanamufuata na kupata maagizo kutoka kwake.
4
Musa alituamuru tutii sheria; ni mali ya taifa letu.
5
Yawe akakuwa mufalme wa Israeli, wakati viongozi wao walipokutana, na makabila yote yalipokusanyika.
6
Musa akasema juu ya kabila la Rubeni: “Rubeni aishi wala asikufe, na watu wake wasikuwe wachache.”
7
Juu ya kabila la Yuda akasema: “Ee Yawe usikilize kilio cha kabila la Yuda; umurudishe tena kwa wandugu zake. Upigane kwa mikono yako kwa ajili yake, usaidie kabila la Yuda mbele ya waadui zake.”
8
Juu ya kabila la Lawi, akasema: “Ee Yawe, upatie wazao wa Lawi shauri lako, shauri lako kwa hao waaminifu wako, ambao uliwajaribu huko Masa. Ulishindana nao kwenye maji ya Meriba.
9
Walawi waliacha wazazi wao, wakawasahau wandugu zao, hawakuwatambua hata watoto wao, maana walifuata amri zako, na kushika agano lako.
10
Na watafundisha wazao wa Yakobo maagizo yako; watafundisha watu wa Israeli sheria yako. Walawi watafukiza ubani mbele yako, sadaka nzima za kuteketezwa juu ya mazabahu yako.
11
Ee Yawe, ubariki nguvu zao, ukubali kazi za mikono yao, uvunje nguvu za waadui zao, nguvu za wanaowachukia hata wasiinuke tena.”
12
Juu ya kabila la Benjamina akasema: “Hili ni kabila Yawe analopenda, nalo linakaa salama karibu naye. Yeye analinda muchana kutwa, na kukaa kati ya milima yake.”
13
Juu ya kabila la Yosefu akasema: “Yawe abariki inchi yake, kwa baraka nzuri kabisa kutoka juu,
14
ibarikiwe kwa matunda bora yanaoiva kwa jua, kwa matunda ya kila mwezi,
15
kwa mazao bora ya milima ya kale, na mazao tele ya milima ya kale.
16
Inchi yake ijae yote yanayokuwa mazuri, ibarikiwe kwa huruma wa Yawe, ambaye alitokea katika kichaka. Baraka hizi zishukie watu wa kabila la Yosefu, aliyekuwa mukubwa kati ya wandugu zake.
17
Utukufu wake ni utukufu wa ngombe dume wa kwanza, pembe zake ni za mbogo dume. Atazitumia kusukuma mataifa; yote atayasukuma mpaka miisho ya dunia. Efuraimu atakuwa na pembe hizo elfu kumi na Manase kwa maelfu.”
18
Juu ya kabila la Zebuluni akasema: “Zebuluni na Isakari mufanikiwe katika shuguli zenu na munapokuwa katika mahema yenu.
19
Watawaalika wageni kwenye milima yao, na huko watu watatolea sadaka. Maana wao watapata utajiri wao kutoka katika bahari na hazina zao katika muchanga wa pembeni ya bahari.”
20
Juu ya kabila la Gadi, akasema: “Atukuzwe Mungu anayemupatia Gadi sehemu kubwa. Gadi anaikaa kama simba akwanyue mukono na mufupa wa kichwa.
21
Alijichagulia eneo zuri kuliko yote, pahali sehemu ya kiongozi ilipotengwa. Aliwaongoza watu na kumutii Yawe, alitimiza mupango wa Mungu kwa Israeli.”
22
Juu ya kabila la Dani akasema hivi: “Dani ni mwana-simba anayeruka kutoka Basani.”
23
Juu ya kabila la Nafutali akasema: “Ee Nafutali uliyeshibishwa upendeleo, uliyejaa baraka za Yawe, inchi yako ni mpaka kwenye ziwa Kinereti na upande wake wa kusini.”
24
Juu ya kabila la Aseri akasema: “Aseri abarikiwe kuliko watoto wote wa Yakobo, na upendelewe na wandugu zako wote; na achovye muguu wake katika mafuta.
25
Miji yako itakuwa ya chuma na shaba. Usalama wako utadumu maisha yako yote!”
26
Musa akamalizia kwa kusema: “Ee Israeli, hakuna anayekuwa kama Mungu wako, yeye anayeruka toka mbinguni kuja kukusaidia, anapita juu katika anga katika utukufu wake.
27
Mungu wa milele ndiye kimbilio lenu; nguvu yake inaonekana katika dunia. Aliwafukuza waadui mbele yenu; aliwaamuru: ‘Muwaangamize.’
28
Kwa hiyo, watu wa Israeli wakakaa salama, wazao wa Yakobo peke yao, katika inchi iliyojaa ngano na divai, inchi ambayo anga lake linadondosha umande.
29
Heri yenu ninyi Waisraeli. Nani anayekuwa kama ninyi, watu muliookolewa na Yawe, ambaye ndiye ngao ya musaada wenu, na upanga unaowaletea ushindi! Waadui zenu watakuja wananyenyekea mbele yenu, nanyi mutawakanyaga chini.”
← Chapter 32
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 34 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34