bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 5
Deuteronomy 5
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 6 →
1
Musa akawaita pamoja Waisraeli, akawaambia: “Enyi Waisraeli, musikilize masharti na maagizo ambayo ninayasema mbele yenu leo. Mujifunze hayo na kuyatimiza kwa uangalifu.
2
Yawe, Mungu wetu, alifanya agano nasi kwenye mulima Horebu.
3
Hakufanya agano hilo na wazee wetu, lakini alilifanya na sisi wote ambao tuko wazima hivi leo.
4
Yawe alisema nanyi kinywa kwa kinywa huko kwenye mulima katikati ya moto.
5
Wakati huo mimi nikasimama kati yenu na Yawe, nikawatangazia yale aliyosema, kwa sababu ninyi muliogopa ule moto na hamukupanda juu ya mulima. Yawe akasema hivi:
6
“Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.
7
“Usikuwe na miungu mingine isipokuwa mimi.
8
“Usijifanyie sanamu za miungu, wala mufano wa kitu chochote kinachokuwa juu mbinguni, wala kinachokuwa chini katika dunia, wala kinachokuwa ndani ya maji chini ya dunia.
9
Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.
10
Lakini ninawatendea mema maelfu ya wale wanaonipenda na kushika amri zangu.
11
“Usitaje bure jina langu mimi Yawe, Mungu wako, maana mimi Yawe sitaacha kumwazibu yeyote anayetaja bure jina langu.
12
“Shika siku ya Sabato na kuitakasa, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru.
13
Siku sita fanya kazi na tenda mambo yako yote.
14
Lakini siku ya saba ni Sabato ya Yawe, Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mutumwa wako, wala mujakazi wako, wala ngombe wako, wala punda wako, wala nyama wako yeyote, wala mugeni anayekuwa katika nyumba yako, kusudi mutumwa wako na mujakazi wako wapate kupumzika vilevile kama vile wewe.
15
Usisahau kwamba wewe ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri, nami Yawe, Mungu wako, nikakutoa huko kwa mukono wenye nguvu na mukono ulionyooshwa. Ndiyo maana mimi Yawe, Mungu wako, nimekuamuru kushika siku ya Sabato.
16
“Uheshimu baba yako na mama yako, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru, kusudi uishi maisha marefu na kufanikiwa katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.
17
“Usiue.
18
“Usizini.
19
“Usiibe.
20
“Usimushuhudie mwenzako uongo.
21
“Usimutamani muke wa mwenzako, wala nyumba yake, wala shamba lake, wala mutumwa wake au mujakazi wake, wala ngombe wake, wala punda wake, wala kitu chochote mwenzako anachokuwa nacho.”
22
“Hizi ndizo amri Yawe alizowaambia ninyi wote kwa sauti kubwa kutoka katika moto na lile wingu zito na giza nene, mulipokuwa mumekusanyika kule kwenye mulima. Hakuongeza hapo amri ingine. Kisha akaandika juu ya vibao viwili vya mawe, akanipatia.
23
“Wakati muliposikia hiyo sauti kutoka katikati ya lile giza, juu ya ule mulima uliokuwa unawaka moto, viongozi wote wa makabila yenu na wazee walinifikia
24
wakasema: ‘Sikiliza! Yawe, Mungu wetu, ametufunulia utukufu na ukubwa wake. Tumeisikia sauti yake kutoka katikati ya ule moto. Leo hivi tumemwona Mungu akisema na mwanadamu, naye mwanadamu pahali pa kufa akaendelea kuishi!
25
Lakini kwa nini kujitia katika hatari ya kufa kwa kuteketezwa na ule moto mukubwa? Tukisikia tena sauti ya Yawe, Mungu wetu tutakufa!
26
Ni mwanadamu gani aliyepata kusikia sauti ya Mungu Mwenye Uzima kutoka katikati ya moto kama vile tulivyomusikia sisi halafu akaweza kubaki muzima?
27
Heri wewe Musa uende karibu, usikilize yote Yawe, Mungu wetu, atakayosema, kisha ukuje kutuambia mambo hayo yote atakayokuambia. Sisi tutayasikiliza na kuyatimiza’.
28
“Bwana akasikia hayo maneno yenu, akaniambia: ‘Nimesikia maneno watu hawa waliyokuambia. Yote waliyosema ni sawa.
29
Heri wangekuwa siku zote na mawazo kama haya wakiniheshimu na kushika amri zangu! Mambo yao yote yangewaendekea vizuri, wao wenyewe na wazao wao milele.
30
Kwenda uwaambie warudi ndani ya mahema yao.
31
Lakini wewe Musa usimame hapa karibu nami. Mimi nitakuambia amri zote na masharti na maagizo ambayo utawafundisha, kusudi inchi ambayo ninawapa ikuwe mali yao.’
32
“Ninyi mukuwe waangalifu mufanye kama vile Yawe alivyowaamuru. Mutimize kila kitu sawasawa.
33
Mutafuata njia yote Yawe, Mungu wenu, aliyowaamuru kufuata kusudi mambo yenu yawaendekee vizuri na mupate kuishi muda murefu katika inchi mutakayotwaa ikuwe mali yenu.
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 6 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34