bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 6
Deuteronomy 6
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 7 →
1
“Hii ndiyo amri, masharti na maagizo ambayo Yawe, Mungu wenu, aliniamuru niwafundishe, kusudi muyatimize katika inchi munayokwenda kuirizi.
2
Wakati wote munapokuwa wazima, mutapaswa kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kutii masharti yote na amri ninazowapa ninyi na wazao wenu kusudi mupate kuishi maisha marefu.
3
Kwa hiyo enyi Waisraeli, mukuwe waangalifu kwa kuzitimiza, kusudi mufanikiwe na kuongezeka sana katika inchi hiyo inayotiririka maziwa na asali kama vile alivyowaahidi.
4
“Basi musikilize, enyi Waisraeli! Yawe, Yawe tu, ni Mungu wetu.
5
Mumupende Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote, kwa roho yenu yote na kwa nguvu yenu yote.
6
Muweke ndani ya moyo wenu maneno hayo ninayowaamuru leo
7
na kuwafundisha kwa uangalifu watoto wenu. Mutawaelezea mutakapokuwa munakaa katika nyumba au munapokuwa katika safari au munapolala au munapoamuka.
8
Muyafunge katika mikono yenu na kuyavaa katika paji za nyuso zenu kama vile ukumbusho.
9
Muyaandike kwenye miimo ya milango yenu na milango ya miji yenu.
10
“Kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo, yeye atawapa inchi yenye miji mikubwa na mizuri iliyostawi ambayo ninyi hamukuijenga.
11
Nyumba zitakuwa zimejaa vitu vizuri ambavyo ninyi hamukuviweka, kutakuwa visima ambavyo hamukuchimba na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hamukuyapanda. Yawe atakapowapeleka kwenye inchi hiyo ambako mutakuwa na chakula chote munachohitaji,
12
muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe aliyewatoa Misri ambako mulikuwa watumwa.
13
Mutamwogopa Yawe, Mungu wenu, mutamutumikia yeye peke yake na kuapa katika jina lake peke yake.
14
Musiabudu miungu mingine, miungu ya watu wanaokuwa jirani nanyi,
15
hasira ya Yawe isiwake juu yenu, naye asiwafute katika dunia, maana Yawe, Mungu wenu, anayekuwa kati yenu, ni Mungu mwenye wivu.
16
“Musimujaribu Yawe, Mungu wenu, kama vile mulivyomujaribu huko Masa.
17
Muhakikishe kwamba munatii amri, maagizo, na masharti ya Yawe, Mungu wenu, ambayo amewaamuru.
18
Mufanye yale yanayomupendeza Yawe, kusudi mupate kufanikiwa. Mutaweza kuirizi inchi ile nzuri ambayo Yawe aliapa kuwapa babu zenu,
19
na mutawafukuza waadui zenu kama vile Yawe alivyoahidi.
20
“Siku zinazokuja, mwana wako atakapokuuliza: ‘Maana ya maagizo, masharti na maamuzi ambayo Yawe, Mungu wetu, aliwaamuru kutenda ni nini?’
21
Ninyi mutawajibu hivi: ‘Sisi tulikuwa watumwa wa mufalme wa Misri, na Yawe akatuokoa kwa mukono wake wenye nguvu.
22
Kwa macho yetu wenyewe tulimwona akifanya vitambulisho na miujiza na mambo ya kutisha na ya ajabu juu ya Wamisri, mufalme wao na wakubwa wake.
23
Alitutoa Misri, akatuleta hapa na kutupa inchi hii, kama vile alivyoapa kwamba atawapa babu zetu.
24
Basi, Yawe akatuamuru kutii masharti haya yote na kumwogopa kwa faida yetu wenyewe, apate kutulinda siku zote kama hivi leo.
25
Tukiwa waangalifu tukitimiza amri zote mbele ya Yawe, Mungu wetu, kama vile alivyotuamuru, tutahesabiwa kuwa wenye haki’.
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 7 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34