bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Genesis 50
Genesis 50
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 49
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
1
Yosefu akamukumbatia baba yake akilia na kumubusu.
2
Kisha, akawaagiza waganga wake wamupakae baba yake Israeli, dawa kusudi asioze, nao wakafanya hivyo.
3
Kama kawaida, siku makumi ine zilihitajika kwa kazi hiyo. Wamisri nao wakaomboleza kifo cha Yakobo kwa muda wa siku makumi saba.
4
Nyuma ya kilio kumalizika, Yosefu akawaambia watu wa jamaa ya mufalme wa Misri: “Ikiwa nimepata kukubaliwa mbele yenu, tafazali muzungumuze na mufalme kwa ajili yangu kwamba baba yangu aliniapisha, akisema:
5
‘Mimi niko karibu kufa. Inakupasa kunizika katika kaburi nililojichongea katika inchi ya Kanana.’ Kwa hiyo ninamwomba aniruhusu niende kumuzika baba yangu, kisha nitarudi.”
6
Mufalme akajibu: “Kwenda umuzike baba yako kama vile alivyokuapisha.”
7
Basi, Yosefu akaondoka kwenda kumuzika baba yake akisindikizwa na watumishi wengi wa mufalme wa Misri, wazee wa nyumba ya mufalme, pamoja na wazee wa inchi nzima ya Misri.
8
Vilevile, Yosefu alisindikizwa na jamaa yake yote, wandugu zake na jamaa yote ya baba yake Yakobo. Katika eneo la Goseni kulibaki watoto wao tu pamoja na kondoo, mbuzi na ngombe wao.
9
Vilevile alisindikizwa na wapanda-farasi na magari, lilikuwa kundi kubwa sana.
10
Walipofika katika uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, ngambo ya muto Yordani, waliomboleza kwa huzuni kubwa, naye Yosefu akamufanyia baba yake marehemu kilio cha siku saba.
11
Wakanana wenyeji wa inchi hiyo, walipoona maombolezo yaliyofanyika kwenye uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, wakasema: “Maombolezo haya ya Wamisri, kweli ni makubwa!” Kwa hiyo, pahali pale pakaitwa Abeli-Misri, napo pako ngambo ya muto Yordani.
12
Wana wa Yakobo walimufanyia baba yao kama vile alivyowaagiza:
13
wakamupeleka mpaka inchi ya Kanana, wakamuzika katika pango lililokuwa katika shamba kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure. Pango pamoja na shamba lile Abrahamu alikuwa amelinunua kwa Efuroni Muhiti, kusudi pakuwe pahali pake pa kuzikia.
14
Nyuma ya kumuzika baba yake, Yosefu akarudi Misri pamoja na wandugu zake na watu wote waliokuwa wakimusindikiza kwenda kumuzika baba yake.
15
Nyuma ya kifo cha baba yao, wandugu za Yosefu walisemezana: “Labda Yosefu atatuchukia na kutulipiza mabaya yote tuliyomutendea.”
16
Kwa hiyo wakamupelekea Yosefu ujumbe, wakisema: “Baba yako, mbele hajakufa, aliagiza hivi:
17
‘Mumwambie Yosefu kwa ajili yangu: Tafazali uwasamehe wandugu zako makosa yao mabaya na maovu yote waliyokutendea.’ Sasa basi, tafazali usamehe uovu tuliokutendea sisi watumishi wa Mungu wa baba yako.” Yosefu alipopata ujumbe huu, akalia.
18
Kisha wandugu zake wakamufikia, wakainama mpaka chini mbele yake, wakasema: “Sisi ni watumishi wako.”
19
Lakini Yosefu akawaambia: “Musiogope, mimi ni pahali pa Mungu?
20
Ninyi mulitaka kunitendea vibaya, lakini Mungu alikusudia mema kusudi watu wengi wapate kuwa wazima kama vile munavyoona leo.
21
Basi, musiogope. Mimi nitawapa chakula pamoja na watoto wenu.” Basi akawafariji na kusema nao vizuri.
22
Yosefu akaendelea kukaa katika inchi ya Misri pamoja na jamaa yote ya baba yake. Aliishi kwa muda wa miaka mia moja na kumi.
23
Yosefu alijaliwa kuwaona watoto na wajukuu wa mwana wake Efuraimu na vilevile kuwapokea kama wana wake watoto wa Makiri mwana wa Manase.
24
Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”
25
Kisha Yosefu akawaapiza wana wa Israeli, akisema: “Mungu atakapowafikia kwa kuwasaidia, muhakikishe kwamba mutapeleka mifupa yangu kutoka huku.”
26
Basi, Yosefu akakufa kule Misri, akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi. Nao wakapakaa mwili wake dawa kusudi usioze, wakauweka katika sanduku kule Misri.
← Chapter 49
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50