bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Jeremiah 2
Jeremiah 2
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 1
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 3 →
1
Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2
Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.
3
Israeli, ulikuwa wangu wa pekee, kama malimbuko ya shamba langu. Wote waliokukula walibeba hukumu, wakipatwa na hasara. –Ni ujumbe wa Yawe.
4
Musikilize neno la Yawe, enyi wazao wa Yakobo. Musikilize, enyi jamaa zote za wazao wa Israeli.
5
Yawe anasema hivi: Babu zenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu ya bure, hata nao wakakuwa watu bure?
6
Hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe aliyetuondoa katika inchi ya Misri, aliyetuongoza katika mbuga, katika inchi ya jangwa na mashimo, inchi inayokauka na yenye giza kubwa, inchi isiyopitiwa na mutu yeyote, wala kukaliwa na mwanadamu?
7
Niliwaleta katika inchi yenye mboleo, muyafurahie mazao yake na mema yake mengine. Lakini mulipofika tu, muliichafua inchi yangu; inchi niliyowapa ikuwe yenu, mukaifanya chukizo.
8
Nao makuhani hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe? Wafundi wa sheria hawakunijua, viongozi wa watu waliniasi; manabii nao walitabiri kwa jina la Bali na kuabudu sanamu zisizokuwa na faida yoyote.
9
Kwa hiyo, mimi nitawashitaki ninyi, na nitawashitaki wazao wenu. –Ni ujumbe wa Yawe.–
10
Basi muvuke bahari mpaka Kipuro, muone, au mutume watu huko Kedari wachunguze, kama jambo kama hili limekwisha kutokea.
11
Kuna taifa ambalo limekwisha kubadilisha miungu yao ingawa miungu hiyo si miungu? Lakini watu wangu wameniacha mimi, utukufu wao, wakafuata miungu isiyokuwa na faida yoyote.
12
Kwa hiyo mushangae, enyi mbingu, muogope na kufazaika kabisa. –Ni ujumbe wa Yawe.–
13
Watu wangu wametenda maovu mawili; wameniacha mimi ninayekuwa chemichemi ya maji ya uzima, wakajichimbia visima vyao wenyewe, visima vyenye nyufa, visivyoweza kuchunga maji.
14
Israeli ni mutumwa, au amezaliwa mutumwa? Hapana! Kwa nini basi amekuwa kama nyama anayewindwa?
15
Simba wananguruma kwa ajili yake, wananguruma kwa sauti kubwa. Wameiharibu kabisa inchi yake, miji yake imebaki mabomoko pasipo watu.
16
Hata watu wa Nofi na Tahapanesi, wamenyoa nywele ya kichwa chake.
17
Israeli, si wewe mwenyewe uliyejiletea hayo yote, kwa kuniacha mimi Yawe, Mungu wako, niliyekuwa ninakuongoza katika njia?
18
Na sasa itakufalia nini kwenda Misri kunywa maji ya muto Nili? Au itakufalia nini kwenda Asuria kunywa maji ya muto Furati?
19
Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–
20
Yawe anasema: Tangu zamani wewe ulivunja nira yako, ulikata minyororo yako, ukasema: “Sitakutumikia”. Juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wa majani mabichi, ukalala machali kama kahaba.
21
Lakini mimi nilikupanda kama mizabibu uliochaguliwa, muzabibu wenye afya na wa mbegu safi. Mbona basi umeharibika, umegeuka kuwa muzabibu wa bure wa pori?
22
Hata ukijisafisha kwa dawa ya kutosha taka na kutumia sabuni nyingi, madoa ya uovu wako yatabaki mbele yangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
23
Namna gani basi unaweza kusema: Mimi sikujichafua wala sikufuata miungu Bali. Ukumbuke vile ulivyotenda zambi kule katika bonde; utambue yale uliyofanya huko! Wewe ni kama mwana wa ngamia, anayetangatanga huko na huko;
24
kama punda dike wa pori aliyezoea jangwa. Katika tamaa yake ananusanusa upepo; nani anayeweza kumuzuiza katika hamu yake? Dume anayemutamani hahitaji kujisumbua; wakati wake unapofika watamupata tu.
25
Israeli, usiichubue miguu yako wala usilikaushe koo lako. Lakini wewe unasema: Hakuna tumaini lolote. Ninapenda miungu ya kigeni, hiyo ndiyo nitakayoifuata.
26
Kama vile mwizi anavyofezeheka anaponaswa, ndivyo Waisraeli watakavyofezeheka; wao wenyewe, wafalme wao, wakubwa wao, makuhani wao na manabii wao.
27
Wao wanauambia muti: “Wewe ni baba yetu”, nalo jiwe: “Wewe ndiwe uliyetuzaa”; kwa maana unanigeuzia mugongo, wala hawakunielekezea uso. Lakini wakati wa shida wanasema: Simama utuokoe!
28
Lakini iko wapi ile miungu yenu muliyojifanyia? Basi kama inaweza, isimame iwasaidie, wakati munapokuwa katika shida. Ee ninyi watu wa Yuda, hesabu ya miungu yenu ni sawa na hesabu ya miji yenu!
29
Kwa nini basi munanilalamikia? Ninyi wote mumeniasi. –Ni ujumbe wa Yawe.–
30
Niliwaazibu ninyi lakini ilikuwa bure, ninyi munakataa maonyo. Muliwateketeza manabii wenu kwa upanga kama simba mwenye uchu.
31
Enyi watu! Musikilize vile mimi Yawe ninavyosema: Nimekuwa kama vile jangwa au inchi yenye giza kubwa? Kwa nini basi watu wangu wanasema: Sisi tuko watu huru; hatutakurudilia!
32
Kijana binti anaweza kusahau mapambo yake, au bibi arusi nguo yake? Lakini watu wangu wamenisahau kwa muda wa siku zisizohesabika.
33
Kweli wewe ni bingwa wa kutafuta wapenzi! Hata wanawake waovu unawafundisha njia zako.
34
Juu ya nguo zako kuna damu ya wamasikini wasiokuwa na kosa, ijapokuwa haukuwakuta wakivunja nyumba yako. Na zaidi ya hayo yote,
35
wewe unasema: Mimi sina kosa; hakika hasira yake imegeuka mbali nami. Lakini mimi nitakuhukumu kwa sababu unasema kwamba haukutenda zambi.
36
Kwa nini unaniachilia hivi, ukibadilishabadilisha mwenendo wako? Utafezeheshwa na Misri kama ulivyofezeheshwa na Asuria.
37
Na huko vilevile utatoka na haya, mikono ikiwa juu ya kichwa. Mimi Yawe nimewakataa wale uliowategemea, wala hautafanikiwa kwa musaada wao.
← Chapter 1
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 3 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52