bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Zechariah 11
Zechariah 11
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 10
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 12 →
1
Fungua milango yako, ewe Lebanoni kusudi moto uiteketeze mierezi yako!
2
Muomboleze, enyi misunobari, kwa sababu mierezi imeteketea. Miti hiyo mitukufu imeharibiwa! Enyi mialo ya Basani, muomboleze, kwa maana pori kubwa limekatwa!
3
Sikia maombolezo ya watawala! Utukufu wao umeharibiwa! Sikia ngurumo za simba! Pori la muto Yordani limeharibiwa!
4
Yawe, Mungu wangu, alisema hivi: Ujifanye muchungaji wa kondoo wanaokwenda kuchinjwa.
5
Wanunuzi wao wanawachinja lakini hawaazibiwi; na wanaowauzisha wanasema: “Yawe ashukuriwe! Sasa tumetajirika.” Hata wachungaji wenyewe hawawaonei huruma.
6
Sitawahurumia tena wakaaji wa dunia. Nitamwacha kila mutu katika mikono ya mwenzake, na kila mwanainchi katika mikono ya mufalme wake. Nao wataiangamiza dunia, nami sitamwokoa mutu yeyote toka katika mikono yao. –Ni ujumbe wa Yawe.
7
Basi, nikakuwa muchungaji wa kondoo ambao wachuuzi waliwatayarisha kwenda kuchinjwa. Nikatwaa fimbo mbili: moja nikaiita “Rehema”, na ingine nikaiita “Umoja”, nikaenda kuchunga kondoo.
8
Kwa muda wa mwezi mumoja, nikaua wachungaji watatu wabaya. Tena uvumilivu wangu kwa kondoo ukaniishia, nao kwa upande wao, wakanichukia.
9
Basi, nikawaambia: “Sitakuwa muchungaji wenu tena. Atakayekufa akufe! Atakayeangamia aangamie! Na wale watakaobaki wakulane wao kwa wao.”
10
Nikakamata ile fimbo yangu niliyoiita “Rehema”, nikaivunja, kuonyesha kwamba agano Yawe alilofanya na watu wake limevunjwa.
11
Na agano hilo likavunjwa siku ileile. Wale wachuuzi wa kondoo waliokuwa wananiangalia, wakajua kwamba neno la Yawe lilikuwa limenifikia.
12
Kisha nikawaambia: Kama mukipendezwa, munilipe mushahara wangu; lakini kama munaona sivyo, basi muache. Basi, wakanipimia vikoroti makumi tatu vya feza kwa mushahara wangu.
13
Kisha Yawe akaniambia: Mushahara huo ni malipo kwa kazi yangu? Basi, uzitie katika hazina ya hekalu. Hivyo nikatwaa hivyo vikoroti makumi tatu vya feza, nikavitia katika hazina ya hekalu la Yawe.
14
Kisha nikavunja ile fimbo yangu ya pili niliyoiita “Umoja” na hivyo nikauvunja umoja kati ya Yuda na Israeli.
15
Yawe akaniambia tena: Ujifanye tena kuwa muchungaji, lakini mara hii ukuwe kama muchungaji mupumbafu!
16
Maana nitaleta katika inchi muchungaji asiyemujali kondoo anayeangamia, au kumutafuta kondoo anayetangatanga, au kumutunza aliyeumizwa wala kumukulisha yule anayekuwa muzima: lakini atakula wale kondoo wanono, hata kwato zao.
17
Ole wake muchungaji mupumbafu, ambaye anawaachilia kondoo wake! Upanga uukate mukono wake, na jicho lake la kuume liongolewe! Mukono wake upooze, jicho lake la kuume lipofuke.
← Chapter 10
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 12 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14