bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
/
Proverbs 3
Proverbs 3
Swahili NMM (Neno: Maandiko Matakatifu) 2018
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 4 →
1
Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
2
kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
3
Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
4
Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
5
Mtumaini bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6
katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
7
Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche bwana ukajiepushe na uovu.
8
Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
9
Mheshimu bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
10
ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
11
Mwanangu, usiidharau adhabu ya bwana na usichukie kukaripiwa naye,
12
kwa sababu bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
13
Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
14
kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
15
Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
16
Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
17
Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
18
Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
19
Kwa hekima bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
20
kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
21
Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
22
ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
23
Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
24
ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
25
Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
26
kwa kuwa bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
27
Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
28
Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
29
Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
30
Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
31
Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
32
kwa kuwa bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
33
Laana ya bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
34
Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
35
Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 4 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31