bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
/
Ruth 4
Ruth 4
Swahili SRB37 (Swahili Roehl Bible 1937)
← Chapter 3
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
1
Boazi akapanda kwenda langoni pa mji, akakaa huko. Mara yule mwingiliaji, Boazi aliyemtaja, akapita; ndipo, alipomwambia: Njoo, wewe bwana fulani, ukae hapa! Akaacha kwenda, akaja kukaa.
2
Kisha akachukua watu kumi walio wazee wa mjini, akawaambia: Kaeni hapa! Nao wakakaa.
3
Akamwambia huyo mwingiliaji: Fungu la shamba lililokuwa lake ndugu yetu Elimeleki, Naomi aliyerudi kutoka kwenye mbuga za Moabu anataka kuliuza.
4
Nami nimesema, niyaeleze masikioni pako kwamba: Linunue machoni pao wanaokaa hapa napo machoni pao wazee wa ukoo wangu! Kama unataka kulikomboa, haya! Likomboe! Kama hutaki kulikomboa, niambie, nijue! Kwani kuliko wewe hakuna awezaye kulikomboa, mimi mwenyewe ni nyuma yako. Akasema: Basi, mimi nitalikomboa.
5
Boazi akamwambia: Siku, utakapolinunua hilo shamba mkononi mwa Naomi na mwa Ruti wa Moabu, umempata naye huyo mke wake yeye aliyekufa, ulikalishe jina lake aliyekufa katika fungu lake.
6
Ndipo, yule mwingiliaji aliposema: Sitaweza kulikomboa, liwe langu, nisiliharibu fungu langu. Likomboe wewe, liwe lako lililonipasa mimi, nilikomboe. Kwani siwezi kulikomboa.
7
Tena kale kwa Waisiraeli ilikuwa desturi, walipokomboa, au waliponunua shamba, wakitaka kulishupaza hilo jambo la namna hii, mtu avue kiatu chake kimoja, ampe mwenzake; huu ulikuwa ushuhuda kwao Waisiraeli.
8
Kwa hiyo, yule mwingiliaji alipomwambia Boazi: Linunue, liwe lako! akakivua kiatu chake.
9
Ndipo, Boazi alipowaambia wale wazee nao watu wote: Ninyi m mashahidi leo hivi, ya kuwa nimeyapata mkononi mwa Naomi yote yaliyokuwa yake Elimeleki nayo yote yaliyokuwa ya Kilioni na ya Maloni.
10
Naye Ruti wa Moabu, mkewe Maloni, nimempata, awe mke wangu, nilikalishe jina lake aliyekufa katika fungu lake, hilo jina lake aliyekufa lisiangamie kwa ndugu zake wala malangoni mahali pake, alipokuwa. Ninyi m mashahidi leo hivi.
11
Ndipo, watu wote waliokuwako malangoni nao wazee wale waliposema: Tu mashahidi. Bwana na amfanye huyu mwanamke aliyeingia nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea walioijenga wote wawili nyumba ya Isiraeli! Pata nguvu mle Efurata, jina lako litajwe mle Beti-Lehemu!
12
Nao mlango wako uwe kama mlango wa Peresi, Tamari aliyemzalia Yuda, nao utoke katika wazao, Bwana atakaokupa kwa kijana huyu!
13
Ndivyo, Boazi alivyomchukua Ruti, akawa mkewe, akaingia nyumbani mwake, Bwana akampa kuwa mwenye mimba, akazaa mtoto wa kiume.
14
Ndipo, wanawake walipomwambia Naomi: Bwana na atukuzwe, kwa kuwa hakukuacha leo, ukose mwingiliaji. Jina lake huyu na litangazwe kwao Waisiraeli,
15
naye na akutulize roho yako kwa kukutunza vema katika uzee wako. Kwani mkweo anayekupenda, akufanyiziaye mema kuliko wana saba wa kiume, ndiye aliyemzaa.
16
Kisha Naomi akamchukua yule mtoto, akamweka kifuani pake, akawa mlezi wake.
17
Nao wanawake wenzake, waliokaa nao, wakamwita jina kwamba: Naomi amezaliwa mwana wa kiume, wakamwita jina lake Obedi (Mtumishi), naye ni babake Isai aliye babake Dawidi.
18
Hawa ndio walio wa uzao wa Peresi: Peresi alimzaa Hesironi,
19
Hesironi akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
20
Aminadabu akamzaa Nasoni, Nasoni akamzaa Salmoni,
21
Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi.
22
Obedi akamzaa Isai, Isai akamzaa Dawidi.
← Chapter 3
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
All chapters:
1
2
3
4