bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Corinthians 16
1 Corinthians 16
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 15
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
1
Sasa juu ya muchango unaofanyika kwa ajili ya watu watakatifu wa Mungu wanaokuwa Yerusalema; ninyi vilevile mufanye sawa vile nilivyoagiza makanisa ya Galatia.
2
Kila siku ya kwanza ya juma, kila mumoja wenu anapaswa kuweka akiba ya mali kwake, kwa kadiri ya mapato yake, kusudi musihitaji kufanya muchango wakati nitakapokuja.
3
Nami nitakapofika, nitatuma watu mutakaochagua, pamoja na barua kwa kupeleka zawadi yenu Yerusalema.
4
Ikiwa ni lazima mimi niende vilevile, basi nitasafiri pamoja nao.
5
Nitakuja kwenu kisha kupitia Makedonia kufuatana na mupango wangu wa kupitia kule.
6
Labda nitabakia pamoja nanyi muda kidogo, au tena wakati wote wa mvua kali; kusudi muweze kunisaidia kuendelea pahali popote nitakapokwenda.
7
Kwa maana sitaki kuonana nanyi kwa kupita tu. Ninatumaini kukaa pamoja nanyi siku chache Bwana akitaka.
8
Lakini, ninataka kubakia hapa Efeso, mpaka siku ya Pentekoste.
9
Kwa maana nimepata hapa wakati muzuri wa kufanya kazi kubwa ijapokuwa wapinzani ni wengi.
10
Kama Timoteo akifika, mujikaze kumupokea vizuri kati yenu kwa sababu yeye anafanya kazi ya Bwana kama mimi mwenyewe.
11
Basi hata mutu mumoja asimuzarau. Lakini mumusaidie aendelee na safari yake katika amani; kusudi apate kurudia kwangu, maana ninamungojea yeye pamoja na wandugu waamini.
12
Kwa ngambo ya ndugu yetu Apolo, nimemusihi sana akuje kwenu pamoja na wandugu wengine, lakini hakutaka kabisa kwenda sasa; atakwenda kwa wakati utakaomupendeza.
13
Mukeshe, musimame imara katika imani, mukuwe hodari na wenye nguvu.
14
Mutende mambo yenu yote katika upendo.
15
Ninyi munajua Stefana na jamaa yake; munafahamu kwamba walikuwa watu wa kwanza walioamini katika inchi ya Akaya, nao wamejitoa kwa kutumikia watu wa Mungu. Hivi ninawasihi sana wandugu zangu,
16
mukubali kuongozwa na watu kama hawa na wale wote wanaotumika na bidii pamoja nao.
17
Nami ninafurahi kwa kufika kwa Stefana, Fortunato na Akaiko; wamekuwa kwa pahali penu,
18
nao wamenifariji kama vile walivyowafariji ninyi wenyewe. Inafaa kuwakumbuka watu kama hawa.
19
Makanisa ya jimbo la Azia yanawasalimia. Akila na Prisila pamoja na kanisa linalokusanyika ndani ya nyumba yao wanawasalimia sana katika Bwana.
20
Wandugu wote wanaokuwa hapa wanawasalimia. Na ninyi vilevile musalimiane kwa upendo wa kikristo.
21
Hii ni salamu ninayoiandika kwa mukono wangu mimi Paulo mwenyewe.
22
Kama mutu hamupendi Bwana, alaaniwe! Bwana wetu, kuja!
23
Neema ya Bwana Yesu ikuwe pamoja nanyi.
24
Ninawapenda ninyi wote katika kuungana na Yesu Kristo.
← Chapter 15
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16