bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
1 Kings 17
1 Kings 17
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 16
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 18 →
1
Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”
2
Kisha, neno la Yawe lilimufikia Elia kusema hivi:
3
“Ondoka hapa uelekee upande wa mashariki, ujifiche kwenye kijito cha Keriti kinachokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani.
4
Kule, utapata maji ya kunywa katika kijito kile. Tena nimewaamuru vibombobombo wakuletee chakula.”
5
Basi, Elia akatii agizo la Yawe, akaenda kukaa kwenye kijito cha Keriti kinachokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani.
6
Vibombobombo wakakuwa wanamuletea mukate na nyama, asubui na magaribi; akapata na maji ya kunywa katika kijito kile.
7
Lakini, nyuma ya siku chache kijito kikakauka kwa sababu hakukunyesha mvua katika inchi.
8
Hapo, neno la Yawe lilimufikia Elia kusema hivi:
9
“Ondoka uende katika muji wa Zerepata, karibu na Sidona, ukae kule. Nimemwamuru mujane mumoja akupatie chakula kule.”
10
Basi, Elia akaondoka, akaenda Zerepata. Alipofika kwenye mulango wa muji, akamukuta mwanamuke mumoja mujane akiokota kuni. Elia akamwita mwanamuke huyo na kumwambia: “Uniletee maji nikunywe.”
11
Yule mwanamuke alipokuwa anaondoka, Elia akamwita tena na kumwambia: “Uniletee na kipande cha mukate vilevile.”
12
Huyo mwanamuke akamwambia: “Kama vile Yawe Mungu wako anavyoishi, sina mukate hata kidogo. Niko tu na unga unaoweza kujaa mukono mumoja katika chungu na mafuta kidogo katika chupa. Nimefika hapa kuokota kuni, kisha niende kwangu kupika chakula hicho, mwana wangu na mimi tukule, kisha tungojee kufa.”
13
Elia akamwambia: “Usiogope. Kwenda ufanye kama vile ulivyosema. Lakini unitengenezee mimi kwanza na kuniletea andazi dogo, kisha ujitengenezee wewe na mwana wako chakula.
14
Maana, Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Unga unaokuwa ndani ya chungu chako hautapunguka wala mafuta yanayokuwa ndani ya chupa hayatakwisha, mpaka pale mimi Yawe nitakaponyesha mvua katika inchi.’ ”
15
Basi, yule mwanamuke mujane akaenda akafanya kama vile alivyoambiwa na Elia hata mama huyo, jamaa yake na Elia wakapata chakula kwa siku nyingi.
16
Unga ndani ya chungu haukupunguka, wala mafuta katika chupa hayakuisha sawa kabisa na neno la Yawe alilomwambia Elia aseme.
17
Nyuma ya hayo, mwana wa mwanamuke huyo mwenye nyumba akagonjwa, na hali yake ikazidi kuwa mbaya, hata kwa mwisho akakufa.
18
Yule mwanamuke akamwambia Elia: “Ewe mutu wa Mungu, kuna maneno gani kati yako nami? Kumbe ulikuja kwangu kwa kuzifichua zambi zangu na kusababisha kifo cha mwana wangu?”
19
Elia akamwambia: “Unipe mwana wako.” Basi, Elia akamutwaa mutoto toka kifua cha mama yake, akamupeleka juu katika chumba chake, akamulalisha juu ya kitanda chake.
20
Kisha akamusihi Yawe akisema: “Ee Yawe, Mungu wangu, hata mwanamuke huyu mujane ambaye ninakaa kwake, naye ananitunza, unamuletea hasara kwa kumwua mwana wake?”
21
Kisha Elia akajinyoosha juu ya mutoto yule mara tatu na kumwomba Yawe: “Ee Yawe, Mungu wangu, umurudishie mutoto huyu roho yake!”
22
Yawe akasikiliza ombi la Elia. Mutoto akaanza kupumua tena.
23
Elia akamurudisha mutoto chini kwa mama yake, akamwambia: “Angalia! Mwana wako yuko muzima.”
24
Huyo mwanamuke mujane akamwambia Elia: “Sasa ninajua kwa hakika kwamba wewe ni mutu wa Mungu, na maneno Yawe aliyokupa uyaseme ni ya kweli.”
← Chapter 16
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 18 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22